Baba Mtakatifu Benedikto XVI, amepeleka salaam zake za pongezi kwa Patriaki mpya wa
Kanisa la Kikoptik la Kiothodox la Alexandria na upatriaki wote wa Jimbo Takatifu
la Mtakatifu Marko, aliyechaguliwa Jumapili iliyopita. . Katika salaam hizo,
Papa Benedikto XV1, ameahidi kushirikiana na Kiongozi huyo mpya, aliyemwombea pia
neema na baraka nyingi za Mwenyezi Mungu, ziweze kumwongoza katika kazi yake mpya
atakayo ianza hivi karibuni. Na ameonyesha imani yake kwamba, atarithi mema yote
yaliyoanzishwa na mtagulizi wake Papa Shenouda III, katika kuwa kiongozi wa kweli
wa kiroho kwa watu wake na mshiriki aminifu, kwa raia wenzake katika kulijenga taifa
jipya la Misri, kwa amani na maridhiano, na kwa ajili ya manufaa ya watu wote wa Mashariki
ya kati .
Papa Benedikto ameendelea kusema, katika nyakati hizi zilizojaa
changamoto, ni muhimu kwa Wakristu wote kuungana na kutolea shuhuda kwa upendo na
usharika unaowaunganisha wote, kupitia utendaji, kama alivyoomba Bwana wakati wa karamu
ya mwisho:ili wote waweze kuwa wamoja , ili dunia isadiki .
Na amemshukuru
Mungu kwa hatua muhimu zilizopigwa , chini ya uongozi wa mtagulizi wake Papa Shenouda
, katika ujenzi wa mahusiano mazuri kati ya Kanisa la Kikoptik la Kiotodosi na Kanisa
Katoliki , na pia katika uaminifu wa tumaini na sala wanazoendelea kuzitolea kwa kwa
ajili ya urafiki na majadiliano, yanayoongozwa na Roho Mtakatifu , kwamba, yataweza
kuzaa matunda ya mshikamano wa karibu zaidi na mapatano ya kudumu.
Mungu wetu
Baba Mbinguni na akujaze amani na nguvu kwa ajili ya kazi hii muhimu inayokusbiri.
Vivyo hivyo , wana siasa na maofisa wa serikali kadhaa wa Misri waonyesha
kufurahia kuchaguliwa kwa Askofu Tawadros, Askofu Msaidizi wa Beheria , kuwa Patriaki
mpya wa kanisa la Kikoputiki la Kiotodosi la Misri, kuchukua nafasi ya Marehemu Shenouda
III.
Uchaguzi huo , ulifanyika Jumapili iliyopita, ambamo jina la Askofu Anba
Tawadros, lilichukuliwa mtoto kati ya vikaratasi vya majina, vilivyokuwa pamoja
kisadukuni, baada ya Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la kikoptiki la Mjini Cairo.
Waziri Mkuu wa Misri Hisham Kandil , pia ametoa pongezi zake kwa Wakoptic
wote kupitia njia ya facebook kwa Papa Tawadros kuchaguliwa, akisema, ni heshima ya
kitaifa,na historia ya Kanisa la Misri. Vivyo hivyo , viongozi wa kijeshi na maofisa
wengine wametoa pia pongezi zao kwa uchaguzi huu .
Askofu Tawadros mwenye
umri wa miaka 60, anakuwa ni Patriaki wa 118, na wa kwanza katika enzi ya utawala
wa serikali inayoongozwa na Chama cha Kisiasa cha udugu wa kiislamu, ambacho kimeonyesha
kufurahia pia kuchaguliwa kwa Tawadros.
Askofu Barnaba el Soryany , wa jijmbo
la kikoptic la Kiotodosi la Mtakatifu George hapa Roma, katika mahojiano baada ya
uchaguzi huo, amemtaja Papa mpya Tawadros , kuwa mtu makini katika utendaji kwa ajili
ya kanisa lake na hasa Misri. Na hivyo kuchaguliwa kwake ni zawadi kubwa kwa kanisa
na watu wote wenye mapenzi mema. Na hivyo wanatazamia kwamba atatembea katika mjia
iliyoachwa na Marehemu Papa Shenouda III, kuwaongoza wana wake kiroho. Na hivyo wanauchukulia
uchaguzi huo kuwa ni uteuzi wa Mungu.