2012-10-27 15:05:22

Tahariri ya Padre Federico Lombardi ...


Licha ya vipingamizi na changamoto nyingi zinazo onekana duniani dhidi ya imani, Mungu bado anaipenda dunia.

Padre Federico Lombardi, ameeleza katika tahariri yake ya wiki hii, akitazama kwa makini, tafakari za Kanisa, juu ya haja ya uinjilishaji mpya, katika dunia ya leo, ambamo mnaonekana watu wengi , kuwa na mwelekeo wa kutaka kujitenga na imani kwa Mungu. Pia mnamo onekana kuwa na vipingamizi na changamoto nyingi zinazo pambana na utangazaji wa Injili, katika maeneo mbalimbali duniani, katika nyakati hizi .

Padre Fedrico Lombardi amerejea Ujumbe wa Sinodi ya Maaskofu uliotolewa kabla ya sinodi hiyo kufungwa, unaolitaka kanisa kutokatatamaa bali, lijitokeza kwa ushupavu kuhubiri Injili ya upendo wa Mungu kwa watu, likiwa limesimama imara katika imani yake kwa Mungu, kwa nguvu za ushuhuda hai wa Kristo Mfufuka na Roho wake.

Na kwamba, hakuna sababu za kuyaona yote kuwa batili katika utandawazi,malimwengu na matukio mapya ya jamii, likiwemo wimbi la uhamiaji. Badala yake vyote hivyo vinapaswa kuchukuliwa na Kanisa kama fursa za uinjilishaji.

Na vipengere vingi vilivyowasilishwa katika majadiliano ya Sinodi ya Maaskofu waliokusanyika kutoka pande mbalimbali za dunia, juu ya ufanyaji upya Kanisa katika maisha ya familia, parokia, Makleri na walei, ni kutokana na utambuzi kwamba, ni utume wa Kanisa kwa familia ya binadamu.

Kanisa daima katika majadiliano juu ya ulimwengu na matatizo yake, katika mitazamo ya tamaduni, sayansi, elimu, sanaa, huduma , pia katika nyanja za uchumi, ajira na siasa, hufanyika kama sehemu ya huduma ya kufanikisha mema kwa wote.

Na kwa namna pekee, ni Kanisa hulenga kujenga ushirikiano na waumini wa dini nyingine, na katika ukweli kwamba, Kanisa haliwezi kujitenga lenyewe, kama kisiwa, bali linapaswa kuuishi imani yake kwa uaminifu ndani ya jamii, mchanganyiko, likiendelea na kazi yake ya kutolea sala na sadaka, na kutambua uwepo wa Mungu kupitia watu wahitaji maskini na fukara wa kiroho.

Padre Federico Lombardi amemalizia tahariri yake kwa kutazama utume wa Maaskofu, katika mazingira yao halisi, kwamba kwa sasa wanaagana na Papa - ambaye kwa uaminifu ameandamana nao katika kazi nzito ya Sinodi , ambamo pia alitoa mchango wake wa kina. Na kwamba, wanatawanyika wakiwa wametiwa nguvu na Mwaka huu wa imani, wakijisikia kuhamasika zaidi katika kutafuta njia , fursa na namna za kuwashirikisha wote, kutangaza uzuri wa imani, yenye thamani zaidi ya vitu vyote vilivyopo.








All the contents on this site are copyrighted ©.