2012-10-26 15:54:39

Papa akutana na Rais wa Cyprus


Mapema Alhamis, Papa alimpokea Rais Demetris Christofias, Rais wa Jamhuri ya Cyprus. Na baadaye Rais huyo alikutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Tarcisio Bertone, akiwa na Katibu wa Mahusiano na Nchi zingine, Askofu Mkuu Domenique Mamberti.
Maongezi ya viongozi hawa yalifanyika katika hali ya urafiki na mazunguzo , yakielnga zaidi katika uimarisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Jimbo la Papa na Jamhuri ya Cyprus. Pia waliweze kuzungumzia mambo yanayogusa nchi zote mbili , na hasa umuhimu wa majadiliano kati ya jamii, na haki za binadamu kuheshimiwa, ikiwemo uhuru wa kidini.
Kwa kuwa Jamhuri ya Cyprus kwa wakati huu ni Rais wa Baraza la Umoja wa Ulaya, pia walitazamisha mawazo yao katika hali za bara la Ulaya kwa wakati huu. Na walionyesha tumaini lao kwamba, , juhudi zinazofanyika kupitia njia za majadiliano,kati ya pande zinazo pingana Mashariki ya kati , hatimaye zitaweza kufanikisha mchango unaofaa kwa jumuiya ya kimataifa kudumisha amani katika eneo hili.








All the contents on this site are copyrighted ©.