2012-10-20 15:49:35

Papa anawaalika Wananchi Mashariki ya Kati kujikita katika kutafuta, kulinda na kudumisha misingi ya amani kwa ajili ya mafao ya wengi!


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, ameonesha masikitiko makubwa kutokana na shambulio la kigaidi lililotokea mjini Beirut, Lebanon, Ijumaa tarehe 19 Oktoba 2012 na kupelekea watu nane kupoteza maisha yao na wengine wengi kupata majeraha.

Baba Mtakatifu ameonesha masikitiko hayo katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Patriaki Bechara Boutros Rai wa Kanisa la Kimaroniti. Baba Mtakatifu anapenda kutumia fursa hii kutoa mwaliko kwa watu wanaoishi huko Mashariki ya Kati kujikita katika mchakato wa kutafuta, kulinda na kudumisha amani kwa ajili ya mafao ya wengi.







All the contents on this site are copyrighted ©.