2012-10-13 15:57:18

Muhtasari wa yaliyojadiliwa katika Sinodi wiki hii


Jumapili hii, inapita wiki moja, tangu Baba Mtakaifu Benedikto XVI, alipozindua Sinodi 13 ya kawaida ya Maaskofu, inayoongozwa na Madambiu: Uinjilishaji Mpya, Uenezaji wa Imani ya Kikristu.

Kwa muhtasari, Mababa wa Sinodi wiki hii, wameweza kusikiliza maelezo , maoni, shuhuda na na uzoefu, juu ya hoja zinazogusa moyo wa kanisa, kama ulegevu wa imani, madhulumu dhidi ya Wakristu na watu maskini, madhulumu ya ngono kwa makundi manyonge, kama watoto na wanawake. Kipeo cha miito ya Upadre na maisha Matakatifu, mahusiano kati ya Sayansi na Imani, umuhimu wa elimu katika jamii, utandawazi na madhara yake na umuhimu wa vyombo vya habari katika katika huduma ya uinjilishaji mpya.

Isabella Piro wa Redio Vatican , akitoa muhtasari huo, ameelelza kwamba, Mababa wa Sinodi , kwa ujumla wamezungumzia nshikamano na umoja wa dini, unaolenga kutobadili nia za dini na kuzuia dini kugeuzwa kuwa uwanja wa Kisiasa. Wasisitiza dini ibaki kuwa chombo cha amani, ni wazo lililotawala majadiliano ya Sinodi siku ya Ijumaa.

Pia sinodi imetazama kashfa za madhulumu ya ngono hasa yanayofanywa na watumishi wa Kanisa wabovu. Maaskofu wamesema kanisa lisiogope kupata habari hizo, na uinjilishaj mpya ni lazima uwakumbatie kafara kwa kuwasikiliza na moyo wa upendo na unyenyekevu, na kutafuta mbinu za kuponya uchungu wa fikira na kurudisha imani yao. Na kwa ajili ya kuzuia na hasa madhulumu kwa watoto , Maaskofu wameshauriana kwamba ni muhimu kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya watoto na makundi dhaifu. Na ili hilo lifanikishwe ni muhimu Kanisa, lifanye mabadiliko katika mifumo yake ya huduma.

Aidha Mababa wa Sinodi wameshirikishana mawazo na uzoefu juu ya kipeo cha imani na kipeo katika maisha ya Kipadre, na hasa wakitazama yanayosababisha uhaba wa miito katika Upadre na maisha yaliyotiwa wakfu, hasa kwa nchi za Magharibi. Hisia za Maaskofu wengi zilielemea katiak kuona kwamba, pengine inatokana na upungufu wa uaminifu kwa wale ambao wameahidi kuushi Ukristu wao kwa kulitumikia kanisa kama Padre au mtawa. Wamesema, kama mhubiri mwenyewe anaonekana kuwa na masiha tofauti na kile anachokihubiri au anachotazamiwa kukishuhudia kimaisha , ni wazi watu hupoteza onjo la kuingia katika maisha hayo.

Pia walisisitiza umuhimu wa kuchagua wenye kuwa na wito wa kweli katika kumtumikia Mungu na Kanisa lake na si zilizofichika zinazolenga kukimbia mambo mengine yanayomzonga mtarajiwa. Wamesema, iwapo ujumbe wa Injili si msingi a imani ya mtu, au si lengo la Padre mwenyewe, basi maisha ya padre huyo ni lazima yatakuwa na kasoro kikanisa.

Hoja ingine iliyotolewa maoni ni suala la umaskini, si umasikini wa mtu lakini pia umasikini wa kiroho , na watu wanaobaguliwa na jamii kutokana na hali yao , kama wagonjwa, wakimbizi, wahamiaji, na wale wanaoitwa walaaniwa. Michango ya Maaskofu katika hili imesema, huu ni wakati kwa Ukristu kutoa jibu linalofaa, lenye kuwakumbatia wote na hasa wanaoishi katika mataifa maskini yanayotafuta kusonga mbele kimaendeleo. Wamesisistiza pia kanisa liwe mstari wa mbele , kusaidia wakimbizi na wahamiaji wanaopambana na kipeo cha kubaguliwa katika hali yoyote ile. Hapo Kanisa ndipo linatakiwa kuiishi Injili ya Msamaria Mwema, katika juhudi hizi za Uinjlishaji mpya.

Bado sinodi ilitazama hoja ya mahusiano kati ya Sayansi na Imani na kuona kwamba, katika ukweli wake mambo hayo hayapingani lakini huinuana, katika kufanikisha ubinadamu zaidi. Lakini wakaonya kwa mara nyingi, kumekuwa na upotoshwaji na kutojali na hivyo kusababisha utengano wa mawazo kati sayannsi nai mani, na kuvionesha kama ni mambo yanayopingana daima, na kumbe kwa kutumiwa vyema ni mambo yanayoinuana. Kwa mtazamo huo, Baraza limeshauri , Mabaraza ya Maaskofu ni muhimu kupambana na hoja za kidharura , kupitia njia ya elimu.

Lakini pia wametahadharisha juu ya shule na vyuo vikuu , zaidi sana Katoliki , kuwekwa chini ya udhibiti wa serikali, na hivyo utendaji wake kushinikizwa na matakwa ya serikali, hata kama hayaendani na imani Katoliki. Na hili limekuwa chanzo kikubwa cha upotoshwaji wa imani ya Mkristu. Na hivyo kunaibuka haja ya kidharura, kwa Kanisa, kujenga majadiliano kati ya imani na tamaduni , majadiliano katika lengo la kuboresha majiundo na shughuli za familia na wahusika wengine katika uwanja wa elimu kama walimu.

Katika mazingira hayo ya utandawazi, Ukumbi wa Sinodi ulionyesha kutambua umuhimu wa mkutano wa watu wa kimataifa ulioanzishwa na Papa, unaofanikishwa na Baraza la Kipapa kwa ajili ya utamaduni , lenye kukuza majadiliano kati ya dini na tamaduni , na watu wasioamini Mungu lakini kindani humtafuta Mungu. Na pia n i muhimu kuwa na majadiliano kati ya dini na hasa mahali ambako wakristu hawawezi kuishuhudia iamani yao , kutokana na hofu za kushambuliwa na waamini wa dini inayowazunguka kama ilivyo katika mataifa kadhaa yenye kuwa na Waislamu wengi.

Sinodi hii inahudhuriwa na Maaskofu kutoka pande zote za dunia , Ulaya 103, Amerika 63, Afrika 50, Asia 39 na Oceania 7, wakiwepo pia wageni maalum waalikwa na watalaam katika nyanja mbalimbali. Sinodi inakamilika tarehe 28 Oktoba 2012









All the contents on this site are copyrighted ©.