Uinjilishaji mpya unapaswa kusimikwa katika mizizi ya makopokeo ya Kanisa-Kardinal
Wuerl
Juhudi Katoliki za kuwafikia waamini wanaosinzia nje ya kanisa, ni muhimu zikaonyesha
umuhimu wa imani leo hii. Na inapaswa kufanyika hivyo, bila ya kupoteza mapokeo msingi
na utambulisho wa imani Katoliki. Kardinali Donald W. Wuerl wa Jimbo Kuu la Washington,
alisema mbele ya Papa Benedict XVI na Mababa wa Sinodi inayoendelea hapa Vatican.
Kardinali Wuerl, ni kati ya walioteuliwa na Papa, kutoa maelezo ya awali ,
katika kazi za Sinodi, kwenye mtazamo mpana wa kimataifa juu ya changamoto za leo
katika uinjilishaji, na maadili yanayotakiwa kama msingi wa kanisa , katika kuwafikia
watu.
Kardinali alisema " tsunami" hii ya malimwengu, imekumba kote, na kuacha
watu na tabia ya ukana Mungu, au kuukataa ukweli kwamba, uwepo wa Mungu ni muhimu
katika kufikiri na utendaji kote kwa binadamu. Na Kazi ya Uinjilishaji mpya ni kuwasaidia
watu kuona kwamba utu na haki za binadamu ni mtiririko kutoka ukweli kwamba , binadamu
wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
"Uinjilishaji mpya lazima kuzungumzia upendo
wa Mungu wa kuokoa kwa watu wote na, wakati huo huo, kutambua kwamba Yesu, ametoa
njia ya wazi na ya kipekee ya ukombozi na wokovu," alisema Kardinali.
Mafundisho
ya kanisa, aliendelea, huthibitisha ukweli wa kile kinachohubiriwa na watu wakati
wakijaribu kushirikishana Injili na wengine na kanisa ni njia ambayo Mungu husambaza
neema zake, hasa kupitai njia za sakramenti.
Kardinali Wuerl aliwaambia wajumbe
wa sinodi, kwamba, katika muda huu wa wiki tatu , wataweza kuangalia kw aukaribu
zaidi kila ya maisha ya kanisa na katika fursa mbalimbali, na pia vikwazo vya uinjilishaji
mpya. Hivyo kazi yao itakuwa ya kujibu kwa "ujasiriā, mshikamano wa kanisa, katika
maana ya dharura na furaha. "
"Kanisa daima linaitwa kwanza kujitafakari lenyewe
. Na kila muumini wake, anapaswa kujiuliza kama anaiisha imani yake kikamilifu kila
siku. Na si swala la maneno lakini kiutendaji.