Benki ya Mkombozi inapania kumkomboa na kumwinua mtanzania katika maisha yake!
Askofu Beatus Kinyaiya, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Mkombozi, inayomilikiwa
na kuendeshwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano maalum na Radio
Vatican anabainishwa kwamba, Benki ya Mkombozi inaendelea kupata mafanikio makubwa
tangu kuanzishwa kwake katika kipindi cha miaka kadhaa iliyopita. Kumekuwepo na ongezeko
kubwa la idadi ya ya watu wanaojiunga na Benkii pamoja na ongezeko la watu wanaowekeza
mitaji yao.
Lengo la Baraza
la Maaskofu kuanzisha Benki ya Mkombozi ni kumwinua mtanzania mwenye kipato cha chini
kwa kumwezesha kwa njia ya mikopo inayopania kumjengea uwezo kiuchumi. Lengo hili
litaweza kufikiwa ikiwa kama kasi ya kupanuka kwa Benki ya Mkombozi itandelea kama
inavyojionesha kwa sasa.
Ni Benki inayojali na kuzingatia maadili ya kazi,
uwajibikaji, nidhamu na uaminifu, daima wafanyakazi wake wakihamasishwa kuchapa kazi
kwa ajili ya mafao na maendeleo ya Tanzania katika ujumla wake.
Taarifa za
Benki ya Mkombozi zinaonesha kwamba, katika kipindi cha mwaka 2011 imejipatia faida
ya kiasi cha shilingi millioni 37. Benki inaendelea kuwahamasisha watanzania kuwekeza
katika Benki hii ili iweze kukuza mtaji wake hadi kufikia kiasi cha shilingi Bilioni
15. Mafanikio ya Benki ya Mkombozi ni kutokana na uadilifu, ufanisi na moyo wa kujituma.
Benki
ya Mkombozi inakabiliana na changamoto mbali mbali katika masuala ya kiteknolojia
pamoja na kuendelea kujipanua sehemu mbali mbali za Tanzania. Wakopaji wanahamasishwa
kuhakikisha kwamba, wanarudisha mikopo yao kadiri ya utaratibu ulioweka ili Benki
ya Mkombozi iendelee kutoa huduma kwa Watanzania wengi zaidi.