2012-10-08 12:54:11

Papa aongoza Ibada ya Misa kwa ajili ya kufungua Sinodi juu ya Uinjilishaji Mpya.


Jumapili hii majira ya asubuhi , Mkutano wa Sinodi ya 13 ya kawaida ya Maaskofu, utakaochukua muda wa wiki tatu hapa Vatican 7-28 Octoba 2012, umefunguliwa na Baba Mtakatifu Benedikto XV1, kwa Ibada ya Misa, iliyofanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.

Ibada ilitanguliwa na sala ya Rosare Takatifu ikisindikizwa na nyimbo za kwaya na maelezo kadhaa ya juu ya mawazo ya Mtakatifu Yohane wa Avila na Mtakatifu Hildegard Bingen waliotajwa kuwa walimu wa Kanisa. Na mwisho wa Rosare kengere zilipigwa, na kutokea mbele ya lango kuu la Kanisa la Mtakatifu Petro, Baba Mtakatifu aliingia kwa maandamano akitanguliwa na Makardinali, Mapatriaki wajumbe wa sinodi, na Maaskofu, kwa ajili ya kuanza Ibada ya Misa.

Baba Mtakatifu, katika mahubiri yake , alilenga zaidi katika mada itakayoongoza Sinodi: Uinjilishaji mpya kwa ajili ya Uenezaji wa Imani ya Kikristu . Alisema mada hii inatazamisha katika mwelekeo wa kimipango kwa maisha ya kanisa , waamini familia , jumuiya na taasisi zake. Mipango inayoleta msukumo wa kufanyika sanjari na kuanza kwa Mwaka wa Imani, hapo tarehe 11 Oktoba 2012, ikienda sambamba na maadhimisho ya miaka hamsini kupita, tangu kuzinduliwa kwa Baraza Pili la Kiekumeni la Vatican, Octoba 1962.

Papa aliwakaribisha na kuwashukuru wajumbe wote wa Sinodi hii aliyoizindua, na kutoa mwaliko kwa waumini , katika muda huu wa wiki tatu zijazo , waisindikize Sinodi kwa sala.

Na akirejea masomo ya Liturujia yaliyosomwa, aliainisha ujumbe wa masomo hayo kwamba, mna vipengere viwili, kwanza ni juu ya ndoa, na jambo la pili ni juu ya Yesu Kristu, Neno wa Mungu, Mtukufu sana, aliyesulubiwa ili wote wapate kuwa na uzima. Hvyo, kwa namna ya kipekee, sinodi hii, itafanyika katika kumtazama sana Yeye katika mwanga wa fumbo lake.

Katika vipindi vyote vya nyakati na mahali, Uinjlishaji daima umekuwa ni juu ya mwanzo wake na mwisho wake, Yesu Kristu Mwana wa Mungu. Na Msalaba ni ishara maalum inayomtambulisha, Yeye anayetajwa katika Injili ; Ishara ya upendo na amani , mwaliko wa uongofu na upatanisho.

Papa kwa maelezo hayo aliwaalika ndugu zake Maaskofu, waanze wao wenyewe kutakatifusha dhamiri zao kwa neema yake.

Papa kwa kifupi, alitafakari juu uinjilishaji mpya, na uhusiano wake na uinjilishaji wa kawaida na kwa mataifa. Alisema, Kanisa lipo kwa ajili ya kuinjilisha. Wanafunzi wa kwanza wa Bwana Yesu Kristo, walitii amri ya mwalimu wao na walikwenda nje , dunia nzima kuitangaza Habari Njema, kueneza jumuiya za Kikristo kila mahali, kama historia ya uinjilishaji inayoonyesha katika vipindi vyote ,wakati watu wa Anglo-Saxon au Slavs, huko Amerika, kazi za misioni Afrika, Asia na Oceania.

Kwa namna hiyo, hata katika nyakati zetu wenyewe, Roho Mtakatifu anaendelea kuwa ndani ya kanisa, akitoa nguvu mpya kwa waamini, kwenda nje na kuihubiri I njili, kulingana na mabadiliko ya nyakati , kama ilivyo elezwa katika waraka wa Mtaguso Mkuu wa pili wa Vatican. Kiinjili, upya huu wa mabadiliko, huzalisha ushawishi kifadhili , kwa namna mbili maalum, kwamba, kwa upande mmoja, ni Utume kwa mataifa, wa kutangaza Injili kwa wale ambao hawana bado kumjua Yesu Kristo na ujumbe wake wa wokovu, na kwa upande mwingine ni Uinjilishaji Mpya, unaoongoza kwa wale ambao, ingawa wamebatizwa, wamejitenga mbali na kanisa au sasa wanaishi nje ya maisha ya Kikristu.

Hivyo Papa alisema, Kikao cha Sinodi iliyofunguliwa, inakuwa ni majitolea kwa uinjilishaji mpya, kusaidia watu watu kukutana na Bwana, ambaye peke ndiye ukamilifu wa maisha na amani; kuigundua imani, kwamba ni chanzo cha neema ambayo huleta furaha na matumaini kwa maisha ya mtu binafsi, familia na jamii kwa ujumla.

Papa ameweka bayana kwamba, ni wazi lengo hili maalum, halipunguzi juhudi za kimisionari katika utendaji wake au shughuli za kawaida za uinjilishaji katika jamii yetu ya Kikristo.








All the contents on this site are copyrighted ©.