2012-10-07 15:03:57

Tujali matendo kuliko maneno -Hayati Kardinali Laurian Rugambwa.


Maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki kutoka ndani na nje ya nchi, walifurika kwa wingi mjini Bukoba kuhudhuria mazishi ya Kardinali wa kwanza Mwafrika, hayati Kardinali Laurian Rugambwa aliyefariki takriban miaka 15 iliyopita, kama tulivyokuwa tayari tunawelezea katika habari zetu na makala zetu.
Itakumbukwa kwamba Kardinali Rugambwa alikuwa mpenzi mkubwa wa mama Bikira Maria na ambaye kikanisa aliiweka Tanzania chini ya usimamizi na mwombezi wa Bikira Maria siku moja kabla ya uhuru wa Tanganyika hapo Desemba nane, na mwezi kama huu mwaka 1997 Kardinali allitwa katika makao ya Bwana kwa pumziko la milele.
Mazishi haya yaliyovuta watu wengine wakiwemo wa madhehebu mbalimbali ya kidini kwani ikumbukwe kuwa tukio hili linaenda sambamba na maadhimisho ya miaka 100 ya kuzaliwa kwa Kardinali huyo pamoja na sherehe za kutabaruku Kanisa Kuu ambalo limekarabatiwa upya chini ya msimamizi wa ‘’Bikira Maria mama wa huruma’’, hivyo ni matukio matatu kwa wakati mmoja ambayo yamefikia kilele katika mwezi wa Bikira Maria.
Taarifa kutoka vyombo vya habari na hasa tulivyoweza kuongea navyo moja kwa moja ni Radio Maria tulielezwa kuwa mitaa yote ilijaa watu katika nyumba zote za kulala wageni, seminari na sehemu nyingine katika familia mbalimbali hili watu wapate kuudhuria tukio hili la kihistoria;Ndugu wapenzi hata katika usalama, hali ya ulinzi iliimarishwa zaidi kuhakikisha utulivu wa mji, hili shughuli za kiroho ziweze kwenda vizuri.
Ibada ya misa iliyanza majira ya saa 5.30 huko Parokia ya Kashozi, iliudhuriwa na maelfu ya watu maaskofu, mapadre, watawa, viongozi mbalimbali wa serikali, wageni kutoka nchi jirani na waamini. Askofu Mkuu wa Jimbo la Mwanza Mwashamu Tadeus Rwahichi aliongoza ibada ya misa .
Ndugu wasilizaji wa Radio Vatikan, tukirudi katika kichwa chetu cha makala yetu ‘tujali matendo kuliko maneno’’
Matendo ndiyo tunaweza kusema ulikuwa moyo wa hayati Rugambwa kwani mengi yamesemwa na mengi yameandikwa kuhusu hayati Rugambwa na hasa katika historia yake,wakati huu ni mwafaka kwetu sisi kuangalia matendo yake, kama wahenga wetu wasemavyo matendo ukidhi aja kuliko maneno, ambayo hata Askofu Tadeus Rwahichi katika omilia yake alisema si katika ‘’porojo au mbwembwe’’.
Kiongozi huyu alitumia uongozi wake kiroho kwa kujali utu wa mwanadamu na ndiyo maana alijali matendo zaidi kuliko kutumia maneno, yaani kuthamini umoja katika madhehebu bila ubaguzi wowote, na kuthamini elimu ya kumpatia maendeleo mtu kwanza.
Taifa lolote linalotaka kuendelea lihaitaji elimu, moyo wa hayati katika utume ilikuwa ni kitu cha kwanza kuhangaikia wote waliokuwa wako tayari kujitoa bila kujibakiza, ni mashahidi wa kutosha katika nyanja zote kuanzia, wito mbalimbali wa mapadre, watawa, madaktari, na watu mbalimbali katika kazi za serikali waliopata msaada kutoka kwake.
Hizo ni juhudi za matendo yake, katika kipaji alichopewa na Mwenyezi Mungu ambapo tunaweza kusema kweli aliweza kuwatumia watu kiroho na kimwili bila kujali kabila, muhimu wenye mapenzi mema na kupenda maendeleo.
Juhudi zake za kuanzisha au kuboresha huduma za afya kama hospitali na zahanati mbalimbali ni mojawapo ya huduma ya kuponya watu mwili na kufariji roho za walio wengi, Kama Yesu mwenyewe alivyofanya katika utume wake na ndivyo alivyo agiza.
Ndugu wikilizaji wa Radio vatikan, hata Askofu mkuu wa jimbo la Mwanza wakati wa ibada yake ya misa jumamosi parokiani Kashozi katika kuelezea utume wa Yesu akiunganisha na utume wa hayati katika enjili ya siku hiyo alionesha kuwa utume wa Yesu ulitekelezwa kwa watu aliokabidhiwa kuwatuliza kiu yao na kuishi kama watu wa Mungu hili wapate kutulizwa kiu hiyo.
Alisema kuwa enjili kama ingeishia katika aya ya 8 ambayo Filipo alimwambia Yesu kuwa awaonyeshe baba yao ingetosha,kwamba hiyo ilikuwa sala kubwa ya kutafakari akitumia neno la kilatini la contemplasio, na kuwa Filipo ni mtangulizi wa hayati Kardinali Rugambwa katika utume, kama kardinali wa tatu wa Afrika na kama askofu wa kwanza wa Afrika ,alitutangulia kumtamani Mungu, alifundisha siyo porojo au mbwembwe bali alifundisha Kristo, alifundisha namna ya kumtafuta, kumjua, kumtumikia na kumpenda Kristo. Alifundisha namna ya kutakatifuza sakramenti za kanisa na alifundisha waliopta fursa ya kumpokea Mungu, ya kuishi uhai wake Kristo; Aliwatawala kama taifa la Mungu wapate kueneza ujumbe wa Mungu.
Askofu Mkuu aliendelea kufafanua kuwa ni kitendo cha kumshukuru Mungu kwa yote aliyomjalia ya kumtoa katika kanisa changa hadi kanisa la ulimwengu , pia kwa vipaji vyake alivyojaliwa akiwa hai, alimwomba Mungu aendelee kuwaita wengi wenye kujaa ari ya kumtangaza Kristo , na wenye kuwa tayari kabisa kujitoa.
Askofu alielezea ni kwanini Hayati Laurean alihamishwa Parokiani Kashozi alikokuwa amezikwa kwa muda, kwani kisheria askofu anazikwa mahali alipohudumu, ila kanisa linaruhusu pia kila askofu kuchagua mahali anapotaka kuzikwa, na hivyo angeweza kuzikwa Dar Es Salaam lakini pia alihudumia kanisa la Rutabo, na akajenga kanisa la Bukoba, na upendeleo wake alitaka apumzike mahali pale, na ndiyo maana mapenzi yake yametimizwa.
Alielezea kwamba ni sehemu aliyotumia vizuri ujana wake , na hivyo masali yake yabaki yakiombewa na kanda yote ya ziwa , kanisa lote la Tanzania na nchi za jirani, lakini pi aliwahasa kuwa wasighafirike kwa kuwa hata mahali alipolazwa si mahali pake, mahali pake ni pale alipomwandalia Kristo hili aweze kufurahi naye katika utukufu wake.
Alimalizia akisema Askofu Thadeus kwamba, Mungu amjalie utukufu pamoja na malaika na watakatifu wote nasi atuombee.








All the contents on this site are copyrighted ©.