2012-10-05 15:16:47

Mkutano wa 13 wa Sinodi kwa ajili ya Uinjilishaji Mpya wawasilishwa rasmi kwa wanahabari


Asubuhi Ijumaa hii octoba 5, 2012, katika ukumbi wa Yohane Paulo 11, jengo la Uchapishaji la Vatican, kuliwasilishwa rasmi kwa wanahabari , Mkutano wa XIII, Sinodi ya Kawaida ya Maaskofu Katoliki. Sinodi hiyo itafanyika mjini Vatican tangu tarehe 7 hadi 28 Octoba 2012, chini ya Mada, Uinjilishaji Mpya: Uenezaji wa Imani ya Kikristu. Uwasilishaji huo uliongozwa na Askofu Mkuu Nikola Eterovic, Katibu Mkuu wa Mkutano huo.

Askofu Mkuu Etrovic akitoa muhtasari wa majadiliano ya Mkutano huo kwamba,ameeleza kwamba, yote yamesimikwa katika maneno ya Yesu Kristu Mwenyewe,”Nendeni Duniani Kote , Mkaitangaze Injili kwa kila Kiumbe” ( Mk 16,15).

Alisema. maneno hayo ya Bwana Yesu Mfufuka, yaliyoandikwa mwishoni mwa Injili ya Mt. Marko, ni msingi wa kazi na Utume wa Kanisa. Ni kwenda kuitangaza habari njema kwa watu wote. Ni agizo la Yesu Kristu, linalo endelea kubaki daima lilelile jana, leo na milele, licha ya mabadiliko ya nyakati au hali za kijami, kitamaduni, kisiasa, na kidini, kama tunavyoziishi sasa.

Ni agizo la kitume kutoka kwa Bwana Mtufufuka, Mshindi wa dhambi na mauti. Na ndilo litakuwa nguvu ya majadiliano yote ya Mkutano wa XIII wa Sinodi ya Maaskofu. Kwa maneno hayo ya Yesu Kristu , na kwa kuzingatia waraka wa kufanyia kazi uliopewa jina "Nyakati za Uinjilishaji Mpya", majadiliano yote yatalenga katika namna ya kufanikisha agizo hilo la Yesu kufika katika kila kaya, kila utamaduni na mazingira.

AskofuMkuu Eterovic pia ameutaja mchakato huu kuwa mgumu na ni i shughuli kubwa kwa Sekretarieti kuu ya Sinodi, hasa kuratibuna kuunganisha maoni na michango ya washiriki.
Kwa ujumla, katika mchakato huu una sura tatu zinazoingiliana, mtazamo wa kiroho, kichungaji na kiteolojia.

Mama Kanisa ameweka tumaini katika sala zilizoanzishwa tangu wakati wa maandalizi ya kazi hii, sala zilizoongezwa nguvu na hija ya Baba Mtakatifu Benedikto XV1, katika madhabahu ya Loreto. Hija ya Alhamis 4 Octoba, ambako alikwenda kuomba msaada wa Mama Maria,ili wajumbe wwangaziwe na kutoa maamuzi yatakayo wezesha kutoa matunda mazuri ya kuineneza Injili ya Kristu ambayo ni Ujume wa upendo.

Na Jumapili 7 Octoba, Baba Mtakatifu Benedikto XV1, ataongoza Ibada ya Misa ya Ekaristi kwa ajili ya ufunguzi wa kazi za Sinodi , ambamo pia Papa atawataja watumishi wawiliwa Mungu, kuwa walimu wa Kanisa, Mtakatifu Giovanni D’Avila na Idelgard di Bingen.








All the contents on this site are copyrighted ©.