2012-09-20 16:11:44

Matembezi ya Kardinali Otunga - mafanikio


Jumamosi iliyopita , mjini Nairobi, kulifanyika “Matembezi ya Harambee ya Kardinali Otunga”,kama ilivyo andaliwa na Jimbo Kuu Katoliki la Nairobi Kenya , kwa lengo la kuchagisha fedha kwa ajili ya ufanikishaji mchakato wa kumtaja Mtumishi wa Mungu Maurice Michael Kardinali Otunga , katika daraja la Wenye Heri. Kati ya wafadhili wa matembezi hayo , ilikuwa ni Benk ya Biashara Kenya(KCB).
Matembezi haya yaliongozwa na Muadhama Kardinali John Njue wa Jimbo Kuu la Nairobi. Wakati huo wa Matembezi, Muadhama Kardinali John Njue aliwaomba waamini na watu wote wenye mapenzi mema, wajitoe kwa ukarimu zaidi, kufanikisha juhudi hizi, kwa kuwa huhitaji fedha nyingi. Na KBC, ilitoa hundi ya shillingi za Kenya , laki moja kwa ajili ya mfuko huu wa Kardinali Otunga.
Na Makamu Msimamizi wa mchakato huo, Bruda Reginald Cruz , akirejea matembezi ya Jumamosi, aliiambia CISA kwamba, watu wengi waliweza kujitokeza kushiriki harambee hii. Na kwamba fedha inayotafutwa ni kwa ajili ya kufanikisha awamu ya kwanza ya mchakato huu, ambayo ni ngazi ya kijimbo. Na tayari wamekwisha fanya shughuli zingine kwa lengo hilo, mfano uwepo wa mashindano ya mpira wa magongo na pia wamekwisha andaa mlo wa jioni .
Matembezi haya yalifungwa wka sala iliyoongozwa na Askofu Mkuu Mstaafu John Jenga wa Jimbo Kuu la la Mombasa, ambaye pia aliwashukuru wote walioshiriki matembezi haya.








All the contents on this site are copyrighted ©.