2012-09-17 15:40:38

Uwepo wa Kanisa iwe ni Ishara ya Amani - asema Papa katika Mkutano wa Kiekumene :


Jumapili majira ya saa kumi za joni, Papa aliuhutubia mkutano wa kiekumene, katika monesteri ya Mama Yetu wa ukombozi ya Charfet, ya Upatriaki Katoliki wa Siro. Mkutano uliohudhuriwa na wawakilishi wa makanisa mbalimbali, na likiwa tukio la mwisho muhimu katika ratiba ya ziara ya Papa Lebanon. Mkutano ulio andaliwa na Patriaki Youssuf Younan, wa Kanisa Katoliki la Siro, katika mtazamo kwamba, ziara hii ya Papa, na iwe chimbuko la kazi za kuleta umoja kamili kwa wafuasi wa Kristu.
Papa akihutubia mkutano huo, Papa alikiri kuona ushuhuda wa imani, unaoendelea kuonekana katika Kanisa Siria ya Antiokia, kama ilivyo katika historia yake tukufu ndefu, yenye kushuhudia upendo motomoto kwa Kristu, ushuhuda ulioleta mhemko wa kuandika nyaraka nyingi za kihistoria, juu ya utendaji wa kishupavu, hata kuyatolea maisha mhanga , wakibaki na imani thabiti mioyoni mwao.

Papa alieleza na kuhimiza kwamba, uwepo wa kanisa uwe kwa ajili ya watu wa mkoa huu kama alama ya amani inayotoka kwa Mungu na pia kama mwanga unaowadumisha katika tumaini hai.

Na kwamba kukutana kwake wajumbe hao, ilikuwa ni ishara inayo onyesha nia thabiti zinazolenga kutoa jibu kwa ombi la Kristu “kwamba wote wawe na Umoja” (Yn 17:21). Papa aliendelea kutaja hali halisi za nyakati hizi ambamo vurugu na ghasia zimepamba moto , akisema, inakuwa ni jambo la muhimu, kwa wafuasi wa Kristu, kutoa shuhuda thabiti katika umoja wao, ili dunia iweze kuusadiki ujumbe wa Kristu, kwamba ni maisha ya upendo , amani na mapatana maridhiano. Wakristu wanapaswa kuona kwamba, katika kuikiri imani na kubatizwa, walichukua dhamana ya kuufika ujumbe huu wa thamani kubwa katika maisha ya watu dunaini kote hasa Mashariki ya Kati.

Papa amewasihi Wakristu wasichoke kuuishi upendo huu wa Kristu , ili hatua kwa hatua waweze kufika katika umoja kamili. Kwa ajili hiyo, Papa alihimiza sala za pamoja na uwajibikaji wa pamoja, na kwa maombezi Mama Bikira Maria kwa Mwanae, waweze kufanikisha nia ili kila binadamu aweze kukombolewa dhidi ya uovu na ghasia, na hivyo Mashariki ya Kati yote maisha ya watu yarudie maridhiano na amani.

Papa alihitimisha na maneno : Nawaachie amani , nawapeni amani yangu(. Yn 14, 27), na yawe maneno na ishara ya kila mmoja inayotolewa katika jina Kristu kwa watu wa mkoa huu mpendwa, katika hamu ya kuona maneno hayo yametimia! Asante!








All the contents on this site are copyrighted ©.