2012-09-17 15:41:35

Jumapili Papa alikamilisha ziara yake ya Kitume ya 24 Kimataifa Lebanon


Baba Mtakatifu Jumapili alikamilisha ziara yake ya siku tatu nchini Lebanon(14-16 Septemba 2012), kwa maneno ya shukurani kwa wenyeji wake na huku akionyesha matumaini ya kurudi tena Mashariki ya kati.

Katika muda huu wa siku tatu , ijumaa hadi Jumapili, alikutana na watu na makundi mbalimbali, viongozi wa kidini na kisiasa na pia lika la vijana, kwao wote akifikisha ujumbe wa amani na mapatano, kama yalivyo mapenzi ya Bwana wetu Yesu Kristu.
Nia nyingine kuu ya ziara hii ilikuwa kukabidhi waraka wake wa kitume , ambao ni matokeo ya sinodi ya Maaskofu maalum, aliyoiitisha Desemba 2010, kujadili hali ya maisha ya Kanisa Mashariki ya Kati.

Papa kabla ya kuianza ziara hii, baadhi ya watazamaji wa mambo walionyesha kuhofia usalama wa Papa kutembelea Mashariki ya Kati , kipindi hiki ambamo kuna mnajitokeza matukio ya ghasia za waislamu wenye siasa kali, kushambulia Wakristu, na migogoro ya kisiasa yeney kusabab isha uwamgajiwa damu .

Papa akizungumza na wanahabari wakati akeilekea Lebanon aliwaambia , pamoja na hali za machafuko na ghasia zinazofanywa kwa wakati huu , hakuwa na wazo la kuifuta ziara hiyo. Alisema, wakati wa hali hizi za wasiwasi mwingi na mashaka,ndiyo unakuwa wakati muafaka wa kukutana na kujadiliana , mbinu za kuondoa hali hizo.

Na wakati akiangana na wenyeji wake katika uwanja wa ndege wa Beirut, Papa alionyesha matumaini yake kwamba, ziara yake imeweza kuionyesha dunia kwamba, inawezekana Wakristu na Waislamu kuishi pamojakwa amani na mshikamano. Na alitoa shukurani zake za dhati kwa Waislamu wote waliofika kumlaki na kumsikiliza, na kufanikisha safari yake.

Na alirudia kukazia wajibu wa Lebanon kwa Mashariki ya Kati, ni kuzidi kushuhudia kwamba, inawezekana wafuasi wa dini , imani na tamaduni mbalimbali kuishi pamoja kwa amani na utulivu. Papa alieleza, akiitaja Lebanon, tangu kale imo katika eneo la madhabahu Matakatifu ya Mungu. Na aliomba Lebanon na watu wake hata leo hii, waendelee, kuishi kwa amani na utulivu , ndani ya eneo hili linalotambulika Kama madhabahu Matakatifu ya Mungu. Papa awasalimia Wakarmalite kabla ya kuelekea Uwanja wa Ndege.

Jumapili , Baba Mtakatifu akielekea Uwanja wa ndege, alisimama kwa muda wa dakika kumi hivi katiak monestri ya Wakarmalite wa Mama wa Mungu, kuwajulia hali na kuwatia shime katika utume wao wa kuwa alama y aumoja na mshikamno nchini Lebabon.

Papa alipokelewa na Mama Mkuu , Tereza wa Mtoto Yesu , mhispania ,ambaye ni kati ya waanzilishi wa nyumba hiyo,waliyoianzishwa miaka 50 iliyopita. Papa alitolea sala katiak jengo dogo la kanisa mahali hapo nakusikiliza wimbo mfupi wa Masista hao. Na aliwabariki na kwuapa zawadi ya Mama Maria akiwa na Mtoto Yesu. Na mwisho alibariki jiwe jipya la msingi litakalowekwa katiak jengo jipya la shirika hilo, linalotazamiwa kujengwa huko Cana Lebanon.








All the contents on this site are copyrighted ©.