2012-09-15 14:01:57

Siku ya kwanza ya ziara ya Papa yafanikiwa - Pd. Lombardi


Mapema Jumamosi, Padre Federico Lombardi, msemaji wa Vatican, akitoa muhtasari wa siku ya kwanza ya ziara ya Papa ameeleza kuwa , siku hiyo ilijaa mikutano mingi na yote ilikwenda vyema. Papa aliweza kutoa jibu la swali la kwanza muhimu katika ziara hii. Jibu lililoweza kutoa wasiwasi na mashaka mengi yaliyokuwepo , kulingana na hali halisi za machafuko yanayojitokeza hapa na pale , ikiwemo mivutano ya kidini katika Mkoa wa Mashariki ya Kati .
Mara kwa mara Papa alirudia kutaja , nia na lengo la ziara yake kwamba ni kupeleka ujumbe amani na kuimarishana katika ujenzi wa amani.
Na kwamba , hotuba ya Papa Uwanja wa Ndege, ililitaja taifa la Lebanon, kuwa mfano kwa mataifa, yenye kuwa na tamaduni na dini mbalimbali, kuweza kuishi pamoja , katika hali ya mshikamano na maelewano .
Na kwa upande wa utume wa Kanisa katika jamii, Papa amesisitiza zaidi wajibu wa walei katika kuwa mashahidi wa amani . Na amehimiza Wakristu kuziishi sheria za nchi na kushiriki shughuli za kitaifa kama ilivyotamkwa katika katiba ya nchi, na kulingana na mafundisho ya Kanisa ya kijamii.
Aidha ametoa wito, kuvishinda vishawishi vyenye kuelekeza katika migawanyiko ya kijamii. Badala yake jamii ijali zaidi kutafauta majawabu kwa njia za mazungumzano na maelewano iwapo panajitokeza hali za kutofautiana kifikra. Na kwamba Ukristu si dhana ya mabavu, bali ni njia ya majadiliano katika ujenzi wa jamii yenye maelewano na mapatano.








All the contents on this site are copyrighted ©.