2012-09-14 10:57:10

Uhuru wa kidini Kimataifa ni sharti msingi kwa ajili ya amani na manufaa ya wote.


Hakikisho la uhuru wa kidini ni dhamana ya maisha adilifu yenye utulivu na amani miongoni mwa jamii . Ni Mchango wa Askofu Mkuu Silvano M. Tomasi, Mtazamaji wa kudumu wa jimbo la Papa katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Geneva , alioutoa siku ya Jumatano, wakati akichangia katika mkutano wa Kimataifa juu ya Uhuru wa Kidini, uliofanyika huko Washington Marekani, kuzungumzia hali halisi za uhuru wa kidini katika nyakati hizi. Amesema uhuru wa kidini sasa ni dharura muhimu leo hii, kama inavyojionyesha wazi pia kwamba, uhuru wa kidini imekuwa ni kati ya hoja zinazo jadiliwa mara kwa mara katika mikutano na midahalo.
AskofuMku Tomasi aliendelea kusema, na ndivyo ilivyo ukweli kwamba, Uhuru wa Kidini, uko katika hali za kugandamizwa duniani. Alieleza kwa kurejea takwimu zinazoonyesha kwamba, asilimia 70% ya watu duniani, wanaishi chini ya mashinikizo ya masharti ya kidini. Zaidi wa watu billioni mbili, ikiwa karibia moja ya tatu ya idadi ya watu duniani , wanaishi katika hali ambazo madhulumu yanazidi kuongezeka, hasa katika miaka ya hivi karibuni, yakionekana mashambulio waziwazi kimwili , uharibifu wa mali na vitu vya kidini.
Pia amekumbusha ni wajibu wa watu wote kuzingatia uhuru wa kidini , kama lengo la kwanza katika utendaji wote wa kila siku. Kwa Wakristu hakuna mjadala katika hilo. Maelezo ya AskofuMkuu Silvano Tomasi aliyaangalisha katika matukio mbalimbali ya kusikitisha katika madhulumu haya kidini, yaliyofanyika hivi karibuni katika mataifa mabalimbali, Nigeria, Kenya Iraki, Siria n.k. yakimfanya mtu atafakari kwa kina suala hili la uhuru wa kidini , na waamini kuheshimiana mmoja kwa mwingine. Na kwamba inavyoonekana mara nyingi madhulumu yamekuwa mabaya zaidi katika mataifa ambako kuna sheria zinazo tetea uhuru wa kidini na hasa sheria inayokataza kashfa dhidi ya mambo ya kidini, sheria hiyo inaonekana kutumika kama kinga ya kudhulumu makundi madogomadogo ya kidini, mfano uwepo wa jumuiya ndogo ya Wakristu katika mataifa yenye kuwa na Waislamu wengi, au pia kundi dogo la Waislamu katika jumuiya nyingine kubwa.
Hotuba ya Mosinyori Tomasi , inaendelea kuangalisha katika hali mbalimbali za mataifa hata uhuru wa kidemokrasia katika mataifa ya Magharibi ambako dini inapenda kuchukuliwa kama ni suala la mtu binafsi, ikisahauliwa kwamba, dini ni chimbuko la uhuru wa kweli wa mtu. Kwa mtazamo huo, kuna mwelekeo wa agenda za kisiasa matokeo yake ni kuwa na uhuru usiokuwa na mipaka na siasa zilizo kinyume na dini. Sheria zisizojali misingi na sheria za maadili katika asili ya binadamu mfano familia na maisha manyoofu matakatifu. Pia kutakana na uhuru huu usiokuwa na mipaka wala uadilifu, vinaendelea hata leo hii, kuendeleza enzi ya watu kufia dini hata katika nyakati zetu.
Kardinali amekumbusha kwamba Mwezi March , Baraza la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya haki za binadamu , lilirudia kwa mara nyingine kutaja azimio linalotetea utetezi wa uhuru wa kidini, kama ilivyokwisha tamkwa tena kwa mara nyingine mwaka 1981 na mwaka 1986, kama kutoa msisitizo wa nguvu katika kuhakikishauhuru wa kidini unaheshimiwa katika ngazi zote tangu kwa mtu binafsi, watu wote kwa ujumla na katika ngazi za kitaasisi na kimataifa.hakikisho la uhuru wa kidini hutoa mchango wake katika dhamana ya kuheshimu tunu za uadilifu, msingi wa uhuru wa kidini kwa kila biandamu. Amesisitiza Askofu Mkuu Silivano Tomasi








All the contents on this site are copyrighted ©.