2012-09-13 15:38:05

Ziara ya Papa Yaiva Lebanon


Baba Mtakatifu Benedikto XV1, mapema Ijumaa hii anaianza safari ya kitume ya 24 Kimataifa kuelekea Lebanon, safari inayolenga kumkutanisha na Kanisa Mashariki ya Kati , ambako pia atatoa waraka wa mwisho wa Sinodi ya Maaskofu ,iliyofanyika Maalum kwa ajili ya Mashariki ya Kati. Hii ni ziara ya siku tatu 14-16 Septemba 2012.
Papa Benedikto XV1,anakuwa ni Papa wa tatu kutembelea Lebanon, akiwa ametanguliwa na Papa Paulo V1 , aliyezuru Lebanon tarehe 2 Desemba 1964 . Na Papa Yohane Paulo 11 aliyetembelea Lebanon tarehe 10-11 May 1997, ambako aliwasilisha hati ya mwisho juu ya Sinodi ya Maaskofu, iliyozungmzia Tumaini Jipya kwa Lebanon.
Ziara ya Papa Benedikto XV1, Lebanon imejengwa katika matumaini ya kuimarisha Kanisa Mashariki ya Kati na kutoa tumaini jipya kwa vijana , na mwamko mpya katika mazungumzano ya kiekumene, na kati ya Waislamu na Wakristu, katika lengo la kuwa na maisha ya amani maelewano na tulivu .
Lebanon, ambayo ina jumuiya ya Wakatoliki ni kubwa, ilichanguliwa tangu mapema, hata kabla Syria haijaingia katika machafuko ya kisiasa, yenye umwagaji wa damu yanayoendelea sasa.
Papa baada ya kukamilisha waraka wa mwisho juu ya Sinodi ya Maaskofu Maalum kwa ajili ya Kanisa la Mashariki, sasa anakwenda kuuwasilisha, , kama matokeo ya sinodi hiyo na utatumika kama mwongozo wa utendaji wa Kanisa Katoliki Mashariki ya Kati. Waraka ambao ni majumuisho ya maoni ya wajumbe waliokutana katika sinodi hii ambayo ilikutanisha wajumbe kutoka jumuiya mbalimbali , si za Kikristu tu lakini pia Waislamu na Wayahudi , kuzitazama hali halisi za maisha ya watu Mashariki ya Kati na hasa wahamiaji na jumuiya ndogondogo za kidini na mtazamo mpana wa kuwa na uhuru kamili na demokrasia. Sinodi hii ilifanyika kabla ya kile kinachoitwa mfumko wa ”Wimbi la Mapambazuko Uarabuni”.
Padre Federico Lombardi hivi karibuni katika tahariri yake ya wiki alisema, kutokana na mabadiliko haya mapya, katika uwanja wa kisiasa katika Mataifa mengi ya Mashariki ya Kati, ni wazi kwa sasa, kumejitokeza hoja ya kidharura katika utume wa Kanisa katika eneo hilo. Hata kama hali ya uinjilishaji inaonekana bado kuwa ngumu zaidi , hivyo, uwepo wa Papa katika eneo hilo, unatumainiwa kuwa msaada mkubwa katika kuvuvia moyo wa mshikamano,amani na utulivu miongoni mwa jamii ya watu wa Mashariki ya kati.
Inaaminika Wakatoliki na Wakristu kwa ujumla , pamoja na uchache wao katika mkoa huo, wanaweza kutoa mchango mkubwa kupitia shuhuda za maisha ya amani na utulivu na ukuzaji wa majadiliano kupitia hali ngumu za mateso wanayoyaishi, na si tu kwa vikundi vya dini zingine vinavyo zidi kuongezeka Mashariki ya kati , lakini pia jumuiya ya kimataifa , kuona umuhimu wa kutoa jibu thabiti katika mivutano ya dunia ya kisiasa, kijiografia au kimikoa.
Papa anakwenda Lebanon , kutoa sauti yake ya matumaini na hamu ya kuwa na amani katika mkoa wa Mashariki ya Kati. Kanisa linatumaini kilio cha Papa kitasikilizwana watu w Mashariki ya katin a jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.
Wakati wa ziara hii ya Papa Lebanon, Jumuiya ya Pax Christ, ina waaalika watu wote, wakati wa siku hizi Papa kutembelea Lebanon, kufanya mafungo na sala kwa nia ya kuombea amani Syria







All the contents on this site are copyrighted ©.