Ujumbe wa Papa kwa Kongamano la Kimataifa la Wakatoliki Walei-
Baba Mtakatifu Benedikto XV1, amepeleka saalaam na ujumbe wa matashi mema kwa
washiriki wa Kongamano la Kimataifa la Wakatoliki Walei Afrika, kupitia kwa Kardinali
Stanslaw Rylko, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Walei. Kongamano
hili la siku tano , 4-9 Septemba 2012, lilifunguliwa Jumanne kwa Ibada ya Misa, mjini
Yaounde Cameroon , na lina hudhuriwa kwa Wakatoliki walei, wakiwepo pia Makardinali,
Maaskofu , Mapadre , na watawa wa kike na kiume. Mkusanyiko huu unaoongozwa na Mada
” Mashahidi wa Yesu Kristu Afrika leo hii: Ninyi ni Chumviya Dunia na Mwanga wa Ulimwengu.
Lengo ni kushirikishana uzoefu wa maisha, katiak dunia ya leo, katiak mtazamo wa kuieneja
Injili ya Upendo wa Kristu kwa watu wote.