Tanzania Mwenyeji wa Mkutano wa Huduma za Kichungaji kwa Wahamiaji Afrika
Warsha ya kwanza kutazama Njia/baraba ya Kichungaji, kwa wahamiaji na watu wasiokuwa
na makazi ya kudumu barani Afrika na Madagascar,itaaanza Jumanne jijini Dar es Salaam
Tanzania . Warsha hii imeandaliwa na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Huduma za Kichungaji
kwa wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi maalum, likishirikiana na Tume mahalia ya
Maaskofu mahalia, kwa ajili ya Huduma za Kichungaji kwa wahamiaji na watu wasiokuwa
na makazi maalum. Warsha hii ya siku tano 11-15 Septemba 2012, inaoongoza
na Mada : Yesu Mwenyewe akatokea , akatembea pamoja nao (Lk24:15).