Maaskofu wapya wapatao 92, kati yao 63 kutoka Afrika , 17 kutoka Asia na 6 kutoka
Amerika ya Kusini na Oceania 6, kwa muda wa wiki mbili , watakuwa na semina yao,
katika Chuo cha Kipapa cha Mtakatifu Paulo hapa Roma. Semina hii , iliyoanza Jumatatu
hii 3 Septemba inaendelea hadi 15 Septemba 2012 , kama ilivyoandaliwa na Shirika
la Kipapa, kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu. Madhumuni ya semina hii,
ni Maaskofu wapya, kupaa ufahamu zaidi juu ya wajibu wa utume wao mpya . Masomo yatatolewa
na maofisa mbalimbali na kutoka Idara mbalimbali za Jimbo la Papa. Siku ya Ijumaa
, watakutana na Baba Mtakatifu katika makazi yake ya wakati wa kiangazi huko Castel
Gandolfo .