Jimbo Kuu la Mwanza lapata Padre mpya - Celestine Nyanda
Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza, Jumatano hii limeongeza jina moja zaidi katika orodha
ya Mapadre wake , baada ya Shemasi Celestine Nyanda , kula kiapo cha kulitumikia kanisa
kwa kuyaishi Matakatifu ya Kipadre. Padre Mpya , Celestine Nyanda alitoa
kiapo hicho katika Ibada ya Misa iliyoongozwa na Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thadei
Ruwa’ich wa Jimbo Kuu la Mwanza, na mbele ya waumini waliofika kushuhudia tukio hili.
Askofu Mkuu Ruwaich katika mahubiri yake , alimsisitiza Padre mpya na Mapadre
kwa ujumla, kuwa manabii wa kweli kama alivyokuwa Nabii Yeremia. Amesema, wito wa
kweli hutoka kw Mungu . Na wito wa kweli ni neema kutoka kwa Mungu.