Baba Mtakatifu Francisko, amepewa zawadi ya picha inayohusu Wito wa Mtume Mathayo.Pia picha hiyo imetengenezwa na wasanii kutoka huko Tifernate huko Perugia nchini Italia. Zawadi hiyo ni kutokana na fursa ya utengenezaji wa Filam moja inayoitwa “Caravaggio, roho na damu” ambayo inahusiana na maisha ya wito wa Mtakatifu Matayo. Baba Mtakatifu amewatia moyo ili waendelee na mpango wa shughuli waliyo ianzisha, na kwamba ni mipango inayopeleka utamaduni wa uzuri katika dunia na kuifanya sanaa iweze kuonekana katika maisha ya binadamu na kwa kila aina kijamii!
Tukio hilo, limefanyika tarehe Jumatano tarehe 30 Mei 2018 asubuhi kabla ya kuanza katekesi yake Baba Mtakatifu ambapo, picha hiyo ilimeletwa na wawakilishi wakuu wa vyombo vya habari, Sky na Vatan, pia hata mwanzilishi wa sanaa Stefano Lazzari ambao kwa pamoja wameshirikiana kutengeneza Filam yenye jina la “Caravaggio, Roho na damu”.
Mhusika wa na mkurugenzi wa Filam ya kisaanii kutoka Shirika la Habari Sky, ameelezea juu ya furaha ya kukutana na Papa Francisko ambaye ameweza kwa ufupi kuelezea juu ya Mtakatifu Matayo wakati akiwa kijana, kwamba alikuwa amebobea katika mambo ya fedha na kuhesabu, lakini akaangazwa na mwanga wa Mungu. Pamoja na hayo Pia mhusika huyo amethibitisha kuwa Filam hiyo imetengenezwa kiufundi kiasi cha kuweza kutoa tafsiri ya picha hiyo ya “Caravaggio, roho na damu” kama alivyo weza kufafanua hata Baba Mtakatifu! Ni shughuli ambayo imetendeka kiufundi kwa ushirikiana wa Sky na Vyombo vya habari Vatican.
Vile vile amekumbusha kuwamba huo ni mkakati ulioanzishwa na vyombo vya Habari na Vatican na Sky tangu 2013, kwa kutoa filam ya kwanza ya kisanii ya Makumbusho Vatican, kwa kushirikiana na uongozi wa Jumba la Makumbusho Vatican; ya pili ilikuwa ni Mtakatifu Petro na Makanisa Makuu ya Papa, Roma, iliyotolewa manmo mwaka 2016 kwa ushirikiano wa vyombo vya habari Vatican, wakati wa kuandaa Jubileo ya Huruma. Na mwaka 2017 wakiwa na uongozi wa Majumba ya makumbusho Vatican, waliweza kutoa filam iitwayo “Taffaello – Mwanzo wa Sanaa”; na nyingine iko katika mchakato wa kutengenezwa ambayo itatolewa mwezi Oktoba yenye jina la Michalengelo- asiye na mwisho”.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |