Tumepokea kwa mshutuko pia maskitiko makubwa ya mashambulizi ya msikiti wa Imam Hussein huko Verulam, Durban na janga kubwa la kuwawa kwa imaman wa msikiti huo na wengine wawili kujeruhiwa. Ndiyo maneno yaliyomo katika ujumbe uliotiwa saini na Askofu Stephen Brislin, Askofu Mkuu wa Cape Town na Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Afrika ya Kusini (SACBC, wakishutumu vikali shambulizi la kigaidi katika msikiti wa kiislam mapema wiki hii katika mji huo.
Askofu Mkuu Brislin kwa niaba ya Kanisa Katoliki Afrika ya Kusini, anatoa salam za rambi rambi kwa wanafamilia na marafiki wa Imam aliye uwawa pia kuwatakia heri na baraka ili wapene kwa haraka wale wote waliojeruhiwa. Katika ujumbe huo unaonesha kuunganika na kusononeka na wanajumuiya wa msikiti wa Imam Hussein,ambao pia umeaharibi vibaya kwa moto na wakati huo kubaki katika sala ya kuwaombea.
Halikadhalika ujumbe unashitumu vikali umwagaji dumu na mashambulizi yasiyo na
maana, wakiomba nguvu za vyombo vya serikali kufanya kazi yake kwa haraka ili kuhakikisha
wanapatikana wahusika hao na kutendewa haki kwa kile walichotenda kwa mujibu wa sheria.
Askofu Brislin anahitimisha, akisema kuwa, uvumilivu wa dini umekuwa ni wa muda mrefu
na wenye tabia ya jamii ya Afrika ya Kusini ambao haukuwahi kumdhuru mwingine na
kwa maana hiy wataendelea kusali kwa ajili ya amani katika nchi yao na dunia nzima,
amani inayojikita juu ya kuheshimu hadhi na haki za kila binadamu.
Kwa mujbu wa shirika la habari za kimisionari Fides, mnamo mnamo 10 Mei baada ya sala
ya saa sita , watu watatu wenye silaha na visu waliingia ndani ya miskiti na baada
ya kuwachoma visu watu watatu , waliwasha moto msikiti huo, Imani alikufa pale pale,
wakati watu wawili walibaki wamejeruhiwa.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |