Jumapili 25 Februari 2018 Baba Mtakatifu Francisko alifanya ziara yake fupi katika Parokia ya Mtakatifu Gelasio I nje kidogo ya mji wa Roma. Wakati wa mahubiri yake anasema; Yesu anajionesha kwa mitume wake jinsi alivyo huko mbinguni, anayeng’aa, anatukuka na mshindi. Anafanya hivyo ili mitume wake waweze kukabiliana na mateso , kashfa ya msalaba, kwa maana wao walikuwa hawajuhi kwamba Yesu anatakufa kama muhalifu, hilo wasingetambua! Anathibitisha.
Walikuwa wanajua kuwa Yesu ni mtawala na ukombozi wa dunia hii kama vile wale watawala ambao wanashinda daima katika mapigano ya vita. Lakini njia ya Yesu ni nyingine; ushindi wa Yesu ni kwa njia ya unyenyekevu katika msalaba. Na kutokana na kwamba jambo hilo lingeonekana la kashfa kwao, Yesu anaamua kuwaonesha ni jambo gani hasa litatokea mara baada ya tukio hilo; ni kitu gani kitawadi baada ya msalaba, lakini pia ni jambo gani tunasubiri hata sisi sote!
Ni utukufu na mbingu hiyo. Ndilo jambo zuri, kwasababu Yesu daima anatuandaa kwa
njia ya majaribu. Kwa namna moja au nyingine lakini ndiyo ujumbe ya kwamba daima anatuandaa.
Anatupatia nguvu za kwenda mbele wakati wa majaribu na kuyashinda kwa nguvu zake.
Yesu hatuachi kamwe peke yetu katika majaribu ya maisha. Anatuandaa na kutusaidia
kama alivyo wandaa mitume wake katika maonesho ya utukufu. Kufanya hivyo mitume watakumbuka
kuchukua msalaba kwa unyenyekevu. Jambo la kwanza la mafundiho ya Kanisa ni kwamba
Yesu anatuandaa daima katika majaribu yanayoendelea na hatuachi peke yetu kamwe!
Jambo la pili ambapo lazima kutambuliwa katika Neno la Mungu, Baba Takatifu Francisko
anasema; “Tazama huyo ndiye mwanangu mpendwa, msikilizeni yeye”. Huo ni ujumbe ambao
Baba wa mbinguni awanawapatia mitume wake. Ujumbe wa Yesu ni kuwaandaa kwa kutazama
utukufu wake; ujumbe wa Baba wa mbinguni unasema“ msikilizeni Yeye. Hakuna kipindi
chochote cha maisha yetu ambacho unaweza kuishi kwa ukamilfu, iwapo husikilizi Yesu.
Baba Mtakatifu anabainisha: Wakati mzuri simama na sikiliza Yesu; wakati mbaya simama
na sikiliza Yesu. Hiyo ndiyo njia! Yeye daima ataelekeza nini la kifanya d. Tuendelee
mbele katika kipindi hiki cha kwaresima kwa mambo mawili: katika majaribu , kukumbuka
utukufu wa Yesu, yaani kile ambacho kinatusubiri. Yesu yupo daima na utukufu wake
kutupatia nguvu . Na kipindi chote cha maisha , sikiliza Yesu anasema nini. Ni katika
Injili, katika Liturujia , daima Yesu anaongea katika mioyo yetu.
Katika maisha yetu ya kila siku labda kuna matatizo au mambo mengi ya kutatua. Lakini vema kutafakari je Yesu anataka kusema nini leo? Jaribu kusikiliza sauti ya Yesu anasema nini ndani ya dhamiri ya moyo. Na kwa njia hiyo ni kufuata ushauri wa Baba yake kuwa “ huyu ndiyo mwanangu mpendwa , msikilizeni Yeye. Atakuwa mama Maria ambaye kwa mujibu wa ushauri wake huko Kana ya Galilaya aliweza kufanya miujiza ya maji kuwa divai. Maria aliwaeleza nini wafuasi wake? “fanyeni atakalowambia. Kwa maana ya kusikiliza Yesu na kufanya kile ambcho anasema, ndiyo njia ya uhakika. Ni kwenda mbele na kumbukumbu ya utukufu wa Yesu na ushauri huo wa kusikiliza na kufanya kile ambacho anasema.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |