2018-02-15 16:35:00

Kalenda ya maelekezo ya maadhimisho ya Papa kwa mwezi machi na Aprili 2018!



Kwa mujibu wa mwandaaji mkuu wa Liturujia za Vatican, Monsinyo Guido Marini ametoa  Kalenda ya maadhimisho ya Baba Mtakatifu Francisko kwa mwezi Machi na Aprili 2018.Tarehe 9 Machi saa 11 jioni masaa ya Ulaya Baba Mtakatifu ataadhimisha liturujia ya kitubio katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Jumamosi 17 Machi, Baba Mtakatifu atafanya ziara yake fupi ya kichungaji kwenda huko Mtakatifu Giovanni Rotondo.

Jumapili tarehe 25 machi,Baba Mtakatifu ataadhimisha  misa katika siku ya Jumapili ya Matawi na mwanzo wa mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo katika uwanja wa Mtakatifu Petro saa 4 asubuhi masaa ya Ulaya. Alhamisi Tarehe 29 Machi  saa 3.30  ataadhimisha Karamu ya mwisho na kubariki mafuta Matakatifu ya Krisma.

Tarehe 30 Machi   Ijumaa Kuu saa 11 jioni, masaa ya Ulaya  Baba Mtakatifu anataadhimisha ibada ya  mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo , katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro na usiku saa 3.15 ataongoza maadhimisho ya njia ya msalaba kuzunguka Magofu ya Colosseo. Jumamosi Kuu tarehe 31 Machi, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro saa 2.30 za usiku masaa ya Ulaya Baba Mtakatifu ataanza mkesha wa Pasaka na kufuatia misa ya Pasaka ya Bwana.
Tarehe 1  Aprili  ni Jumapili ya Pasaka. Katika uwanja wa Mtakatifu Petro saa 4 kamili masaa ya Ulaya, Baba Mtakatifu anataongoza misa ya Sikukuu ya pasaka  na saa sita kamili kufuatia Baraka ya “Urbi et Orbi”


Domenika ya Pili ya Pasaka, tarehe 8 Aprili saa 4.30 masaa ya Ulaya, Baba Mtakatifu ataadhimisha misa Takatifu ikiwa ni sikukuu ya huruma ya Mungu, ambapo itakuwa ni fursa ya wamisionari wa huruma  kukutana na Baba Mtakatifu Francisko.

Sr Angela Rwezaula
Vatican News








All the contents on this site are copyrighted ©.