Mchana wa tarehe 1 Desemba 2017 Baba Mtakatifu amekutana na viongozi wa madhehebu
ya kidini kwa ajili ya amani katika makao makuu ya Askofu wa Dhaka nchini Bangladesh.
Katika hotuba yake, kwa wawakilishi kutoka katika jumuiya mbalimbali za kidini za
nchi hiyo amesema, ni fursa kwa mtazamo wa nchi ya Bangladesh ili kuweza kujikita
katika tafakari ya urafiki wao na kuonesha matashi yao mema hasa ya zawadi ya amani
kamili na ya kudumu.
Shukrani kwa Kardinali D’Rozario kwa hotuba yake, kwa makaribisho ya furaha kwa jina
la jumuiya ya waislam, wahindu, wabudha n,hata kwa viongozi wa madaraka ya kiraia.
Anamshukuru pia Askofu wa Kianglikani wa Dhaka kwa uwepo wake na jumuiya nyingine
za kikristo, wakiwemo hata wadua mbalimbali waliochangia kufanikisha mkutano huo.
Nyimbo na ngoma zilizotumbuizwa anasema, zimewezesha kuchangamsha makutano hayo, ambazo zinajieleza kwa namna ya pekee ya utashi wa umoja, undugu na amani katika mafundisho yaliyomo kwa kila dini duniani. Mkutano huo anaongeza, unaweza kuwa kweli ishara ya juhudi kwa viongozi na wafuasi wa madhehebu mengine ya dini yaliyomo katika nchi hiyo, kuishi kwa pamoja katika kuheshimiana na matashi mema. Nchi ya Bangladesh hawali ya yote ni mahali ambapo haki na uhuru wa dini ni msingi wa kwanza, huo ndiyo wito wa kuheshimu, lakini pia hata kupambana na yule atakayetaka kuzusha mgawanyiko, chuki na vurugu kwa jina la dini.
Ni ishara kubwa ya matumaini katika nyakati zetu, ambazo waamini na watu wenye mapenzi mema wanataka kuitikia katika kushirikiana kwenya mafunzo ya utamaduni wa makutano, mazungumzo na kushirikiana katika huduma ya familia ya kibinadamu. Yote haya yanahitaji hasa uvumilivu wa kweli. Uvumilivu huo unaweza kuwa na tabia ya kuchukuliana kwa pamoja, kuwa na imani, uelewa kwa kujenga umoja na kwa kutambua kuwa utofauti siyo tishio, bali ni nguvu na kisima cha utajiri na kukua kwa pamoja!
Wote wanaalikwa kujenga aina ya ufunguzi na kupanua mioyo, kwa maana ya kuwaona
wengine kama njia ya upamoja na si kama vizingiti.
Baba Mtakatifu akifafanua zaidi juu ya aina msingi ya kufungua mioyo ambayo ni tabia
ya utamaduni wa makutano amesema: hawali ya yote ni kama mlango aambayo siyo wa kutoa
historia za abunuasi, bali ni uzoefu halisi wa kushi. Hiyo inasaidia kutambua vema
mazungumzo ya maisha, si tu kubadilisha mawazo bali uthabiti wa kuishi ki ukweli.
Kwa maana inahitaji utashi mwema wa mpyo katika , kukaribisha, si katika kuchanganya
na tofauti au katika kuelezea kile ambacho unaamini kwa kina. Ni kwa njia ya kujikita
kwa kina kuwa na mwingine, maana yake ni kushirikishana uraia na utofauti wa kidini,na
kiutamaduni, lakini zaidi kwa njia ya unyenyekevu, uaminifu na kuheshimiana. Kwa kufanya
hivyo inakuwa ni ishara wazi ya kchukuliana na kuthaminiana na wengine kwa kila hali
ya maisha ikiwa ni dini, lugha, kabila na yote . Na ndani yake ipo hekima na nguvu
muhimu za kuonesha mshikano kuwasaidia wengine kwa dhati.
Kuwa na moyo uliofunguka ni kujionesha katika kupokea na kukaribisha, kushikishana kati ya waamini na zaidi katika kuchangia kwenye utamaduni wa umoja, maelewano, ambayo ynatoa msukumo ndani ya moyo. Baba Mtakatifu anasisitiza kusema, jinsi gani dunia hii inahitaji moyo unao dunda kwa nguvu ili kipinga virusi vya rushwa kisiasa, itikadi kali za kidini zinazoharibu, vishawishi vya kufunga macho mbele ya mahitaji ya wengine kama vile ya maskini, wahamiaji na makundi madogomadogo ya watu katika ulimwengu, kwa namna ya pekee kwa vijana ambao mara nyingi wanahisi upweke, wakitafuta maana ya kweli ya maisha.
Amemalizia awashukuru kwa jitihada zao za kuhamasisha utamaduni wa makutano na kuomba kuwa, maonesho ya juhudi za pamoja za wafuasi wa dini katika kung’amua mema na kujikita katika vitendo vya dhati ili waweze kuwasaidia waamini wakue kwa hekima na utakatifu, kwa kushirikiana katika ujenzi wa dunia ya kibinadamu na umoja.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |