2017-11-10 15:28:00

Papa:Kama mkristo kweli hepukana na ulaghai na kufanya ufisadi!


Ni historia ya ufisadi wa kila siku, inayoelezwa katika Injili ya Mtakatifu Luka akionesha tajiri aliyekuwa na wakili wake akatapanya mali zake na baada ya kugunduliwa, badala ya kutafuta kazi ya halali, anaendelea kuiba kwa kutumia ujanja kwa wengine. Baba Mtakatifu anaongeza huo ndiyo tunaita kweli ufisadi !

Hayo ni mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Misa ya asubuhi Ijumaa tarehe 10 Novemba 2017 katika Kanisa la Mtakatifu Marta mjini Vatican. Baba Mtakatifu akiendelea na mahubiri yake anasema, hawa ni wenye madaraka wanaoendeleza ufisasi hadi kuwa na tabia za kialifu. Hii ni historia ya halisi na siyo liwaya. Siyo historia ya kutafuta katika vitabu vya kizamani vya kihistori, maana inapatikana kila siku katika magazeti. Haya yanatokea leo hii na hasa kwa walio na madaraka  na usimamizi wa mali za watu, siyo kwa mali binafsi. Hakuna anayefanya ufisadi mali binafsi  badala yake ni  kuitetea, kuilinda mali zao binafsi!

Katika Injili Yesu anatambua wakili mdhalimu na kusema kuwa kuwa, „wana wa ulimwengu huu  katika kizazi chao wenyewe huwa na busara kuliko wana wa nuru”: Baba Mtakatifu anaongeza, huo ni katika ufisadi wao mkubwa, ulaghai wao wa kuelendeleza mbele wakijidai na utafadhali ambao unajitokeza kiujanja ujanja tu… je kwa namna hiyo unaweza kuitwa udhalimu wa kikristo?
Lakini kama hawa ni wadhalimu zaidi ya wakristo, hatuwezi kusema kuwa ni wakristo kwasababu hata mafisadi wengi wanadai ni wakristo, je udhalimu unaingilianaje na imani na Kristo?

Baba Mtakatifu anaendelea na maswali mengi  wakati huo akitafakari  tafakatri na kusema, zipo tabia za watu wanaotaka kumfuata Yesu, ili hatimaye wasishie kuliwa wakiwa wazima , kama alivyokuwa akisema hata mama yake  wakati akiwa mdogo kwamba  „kuwatafuna wakiwa wabichi wengine”. Je ni udhalimu gani wa kikristo ambao hautaishia katika dhambi? Pamoja na kwamba  wapo wengine wanafanya ujanja kila siku wakati wanajiitia wakristo. Akifafanua zaidi, Baba Mtakatifu anaonesha mifano zaidi, hata Yesu alikuwa anawatambua wakristo wadhalimu, na ndiyo maana katika Injili pia inaeleza juu ya wakristo kuwa makini na "mbwa mwitu  na kondoo” au busara kama "nyoka na rahisi kama "jiwa” . Kutokana na mifano hiyo je tufanye nini ? 

Baba Mtakatifu ameelezea tabia tatu za kuishi kikristo  ili kuepukana na udhalimu wa namna hiyo: kwanza kuishi na imani thabiti yaani kuwa makini dhini ya  walaghai wanaokuja wakiahidi uwekezaji wa banki, ili baadaye upate faida mara mbili.

Tabia ya pili anasema, ni ile ya kutafakari mbele ya ulaghai wa shetani anayetambua madhaifu yetu na mwisho tabia ya tatu ni ile ya sala.
Amemalizia akiomba Bwana atujalie neema ya kuwa na busara ya kikristo na kuondokana na udhalimu. Kwa maana ndani ya Maisha ya Mkristo anahifadhi tunu msingi ambayo ni Roho Mtakatifu. Hivyo ni lazima kutunza, la sivyo wajinga wanaibiwa roho hiyo. Mkristo yoyote hasiache aibiwe Roho hiyo na kuruhus  kuwa mpumbavu.

Injiili pia ya leo iwe fursa ya kuwaombea hata  mafisadi wote. Kwa maana anasema mara nyingi  wanazungumza juu ya uchafuzi wa mazingira, lakini hakuna kitu kibaya zaidi pia ya uchafuzi wa jamii utokanao na ufisadi , hivyo amesisitiza kusali zaidi kwa ajili ya hao mafisadi waliofungwa katika gereza la ufisadi walioruhusu wenyewe kuingia.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.