Maaskofu Katoliki nchini Kenya wanaomboleza kifo cha marehemu Askofu Cornelius Arap Korir kilichotokea usiku wa tarehe 29 Oktoba 2017 nyumbani kwake huko Eldoret. Akithibitisha kifo hicho cha ghafla katika jimbo la Eldoret, Mwenyekiti wa KCCB na Askofu wa Homabay Philip Anyolo amesema, Askofu Korir alitakiwa kupelekwa Nairobi kwa matibabu zaidi mnamo tarehe 30 Oktoba 2017. Lakini siku aliyotakiwa kwenda, Padre alipokwenda kumwona hakuwa ameamka. Daktari aliitwa na kuthibitisha kwamba askofu hakuwa tena hai. Kwa upande wao anasema, Kanisa limekumbwa na huzuni sana.
Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 30 Oktoba, 2017 huko Eldoret, Askofu Anyolo alitangaza kuwa Misa Takatifu itafanyika kila siku katika Kanisa la Eldoret kuanzia saa 1.00 mchana masaa ya Afrika ya Masahariki kwa ajili ya marehemu Askofu mpaka hapo atakapopumzishwa katika nyumba yake ya milele. Mpaka alipofikwa na umauti, Askofu Korir alikuwa Mwenyekiti wa Tume Katoliki na Haki ya na Amani ya Baraza la Maaskofu Kenya (KCCB) na Askofu wa Eldoret.
Alijulikana sana kwa nafasi yake katika kutetea amani na kupinga ukiukwaji wa haki
za kijamii na kwa sababu hiyo viongozi wa kidini kutoka jumuiya za madhehebu mengine
chini ya mwavuli wa Kikundi cha Mazungumzo (DRG) ambapo alikuwa pia ni mwenyekiti.
Kikundi hiki kinajumuisha uongozi wa juu kutoka Mkutano wa Baraza la Maaskofu Katoliki
wa Kesnya (KCCB), Halmashauri ya Taifa ya Makanisa nchini Kenya (NCCK), Baraza Kuu
la Waislam wa Kenya (SUPKEM) na Baraza la Viongozi wa Kiislamu (NAMLEF), Baraza la
Hindu Kenya (HCK), Shirikikisho la Kiinjili Kenya (EAK) na Shirika la Makanisa la
Afrika (OAIC), Seventh Day Adventist (SDA) na Shia Ithna-Asheri.
Askofu Korir alizaliwa mnamo tarehe 6, Julai,1950. Alipata daraja la Upadre mwaka
1982 na baadaye akachaguliwa kuwa Askofu Jimbo la Eldoret mnamo tarehe 2 Aprili 1990.
Askofu Korir alikuwa miongoni mwa viongozi wa Kanisa Kaskazini mwa Kenya ambaye amekuwa
akionya viongozi wa kisiasa dhidi ya maneno ambayo yanaweza kuwagawa Wakenya kwa ukabila.
Marehemu Askofu Korir atazikwa Jumamosi, tarehe 11 Novemba 201.
Apumzike kwa amani.
All the contents on this site are copyrighted ©. |