2017-11-06 10:52:00

Baba Mtakatifu akutana na Rais wa Jamhuri ya nchi ya Moldva Bw. Dodon


Jumamosi 4 Novemba 2017, Baba Mtakatifu Francisko amekutana na kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya nchi ya Moldova Bwana Igor Dodon. Na  mara baada ya mkutano huo amekutana na Katibu wa Vatican Kardinali Pietro Parolin, akisindikizana na Makamu Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican Askofu Mkuu Antoine Camilleri.

Katika mazungumzo yao, wamesifu ushirikiano na mahusiano mema yaliyopo baina ya nchi hizo mbili na mchango mkubwa wa Kanisa Katoliki utolewao katika jamii ya Moldava hasa kwa njia ya jitihada za kiekumene na kujikita katika huduma  ya elimu na upendo kwa wahitaji.
Aidha  mazungumzo yao pia yamekuwa ni kubadilisha mawazo juu ya hali halisi ya nchi na mada mbalimbali inayohusu nchi yao ikiwa pamoja na uhamasishaji wa thamani ya familia, amani, usalama kwa ngazi ya kikanda na Kimataifa.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.