Kumbuka Ulaya ambayo haijatengenezwa na namba bali na watu. Wakristo wote wa Ulaya wajenge jamii inayosimama juu ya binadamu na jumuiya. Ni msisitizo wa Baba Mtakatifu katika hotuba yake aliyotoa jioni ya tarehe 28 Oktoba kwenye Mkutano wa Kamati ya Baraza la Maaskofu Ulaya katika mada ya kuifikiria Ulaya. Mkutano umefanyika kwa lengo la maadhimisho ya miaka 60 ya mkataba wa Roma kwa ajili ya Ulaya.
Mchango Mkubwa ambao unaweza kutolewa na wakristo wa Ulaya leo hii ni ule wa utambuzi ya kwamba siyo tu idadi za katiba bali Ulaya imetengenezwa na watu. Ametoa hotuba hiyo kwa washiriki wa Mkutano 350 katika Ukumbi Mpya wa Sinodi wenye kauli mbiu juu ya kufikiria Ulaya. Mchango wa Kikristo katika nyati zijazo za mipango ya Ulaya.
Mkutano huo umeudhuliwa na makardinali, maaskofu, mabalozi na wawakilishi kutoka
katika mashirika ya kikristo, ili kujadili kwa pamoja Mkutano ulioandaliwa na Baraza
la Maaskofu wa Ulaya na Tume ya Kamati ya Jumuiya ya Ulaya. Baba Mtakatifu amewaonesha
njia, kwamba msingi wa Ulya ni watu na jumuiya kama wakristo wanaotaka na ambao wanaweza
kutoa mchango mkubwa na kuijenga Ulaya.
Matofari ni mazungumzo, ushirkishwaji, mshikamano maendeleo na amani. Aidha amekumbusha
kuwa thamani msingi ambayo wakristo wameichukua hadi sasa ni maana ya utu ambao ni
mfano wa Mungu.
Akichambua zaidi, ametoa mfano wa Mtakatifu Benedikto, Baba Mtakatifu anasema, binadamu
siyo tena kuwa ni rahisi kuwa mzalendo au mtumishi wa utawala wa usiku, wala kuwa
bidhaa ya kubadilisha na kuwa kazi. Kwa mtazamo wa Benedikto anasema hakuna kutoa
nafasi hiyi, bali yupo binadamu, lakini kwa bahati mbaya Baba Mtakatifu anaendelea
kusema, leo hii hakuna wafanyakazi wapo wale wanaonesha uchumi, hakuna wahamiaji,
wapo wanaodai fedha, kwa maana wanataka namba tu.
Kuwa na sura inakulazimisha kuwajibika, kwa njia hiyo wakristo wanapaswa kukumbuka
kuwa zaidi ya yote Ulaya ni imetengenezwa na watu ili waweze kugundua maana ya ushiriki
wa jumuiya, na kupinga tabia za kuishi kiupweke, kwa kufikiria kuwa ni mantiki ya
uhuru ambao ni kufanya uishi kipekee. Kwa mujibu wa Baba Mtakatifu anasema, hili
ni jambo la hatari. Wakristo wanatambua utambulisho wao zaidi ni ule wa kujenga familia
ambayo ni msingi na ndiyo sehemu ya kugundua utambulisho huo. Muungano utofauti kati
ya mke na mme ambao kama ni wa kweli, unatoa matunda, na uwezo wa kujifungua maisha
na kwa wengine. Jumuiya hai inatambua kwa dhati kupokea kila aina ya tofauti bila
ubaguzi na kutoa matunda mpya katika, kazi, ubunifu na utamaduni
Kutoka Kaskazini, kusini, mashariki na Magharibi, Ulaya ni lazima iwe sehemu ya mazungumzo
anasema Baba Mtakatifu kama ilivyokuwa zamani, na siyo tu nafasi ya kuichumi bali
moyo wa kisiasa.kwa maana hiyo Baba Mtakatifu anawaalika kufikiria nafasi chanya iliyo
nayo dini katika jamii na kwamba inawezekana mazungumzo ya kidini kati ya wakristo,
waislam Ulaya. Aidha anabainisha hatari zaidi ya mawazo potofu yanayojitokeza juu
ya thamani ya dini katika maisha ya umma. Mara nyingi sauti ya mazungumzo mema ugeuka
kuwa kelele za kulipiza visasi. Na hiyo imejitokeza katika baadhi ya nchi, kwa maana
hiyo wakristo wanaalikwa kukuza mazungumzo ya kisiasa yaliyo mema kwa kutoa hadhi
kisiasa ili iweze kuwa huduma kwa ajili ya mema ya wote.
Akielezea maana ya uongozi pia Baba Mtakatifu anasema, kuwa kiongozi leo hii inahitaji
mafunzo, kujiandaa vema na uzoefu, kwa maana hiyo, Ulaya inapaswa iwenafasi muhimu
ya kutoa thamani ya utofauti, kwa mtazamo wa wahamiaji kwamba ni rasilimali badala
ya kuonekana kuwa ni mzigo wa kutupilia mbali. Kwa upande mwingine anasema viongozi
wanapaswa kuwa makini katika suala linalohusu uhamiaji, kwa maana hiyo, wasijenge
kamwe kuta bali mchakato ambao pia unatoa sheria. Na kwa upande wa wahamiaji lazima
wafuate na kuheshimu sheria na kukubali utamaduni wa nchi inayowapokea. Kujikita kwa
ajili ya jumuiya inayoshirikiana maana yake ni ujenzi wa nafasi ya mshikamano na siyo
tu upamoja wa vikundi vidogo vya kujinufaisha.
Ni lazima kuwa na ukarimu kwa wadhaifu na kuwasaidia kizazi kijacho. Tangu miaka
ya 60 migogoro ya kizazi inaendelea bila kukosa, anabainisha na kueleza, siyo tu kwa
upande wa Ulaya kukosa watoto bali wengi wa watoto wamenyimwa haki ya kuzaliwa kwasababu
pia kugundua uweze wa kukabidhi vijana nyenzo na utamaduni wa kukkìabiliana na wakati
endelevu. Ulaya inaishi kwa namna nyingine kwa ukosefu wa kumbukumbu, kwa njia hiyo
inapaswa kugunda thamnai ya wakati uliopita, ili kutajilisha wakati uliopo na kuwakabidhi
kizazi kijacho matumaini. Vijana wengi wanajikuta wamepotea njia mbele ya ukosefu
mizizi na upeo, wakati huo huo elimu inapaswa kujikita katika jumuiya nzima
Ulaya inaitwa kuwa chemi chemi ya maendeleo kamili kama vile alivyokuwa anafikiria
Mwenye heri Papa Paulo VI: Inahitajikita kazi na hali inayostahili katika kazi. Mfano
unaweza kuwa kwa wakristo waajili ambao kwa karne iliyopita walianzisha makampuni
ili kuweza kutoa ajira yenye hadhi kazini; kuanzisha kwake hata leo hii inahitajika
katika ulimwengu wa utandawazi usiokuwa na roho, ambao umeunda magunia mengi ya unyonyaji
na umasikini. Hii inahitaji watawala wa nchi wa kuweza kuanzisha mzunguko wa fadhila
hii, anaongeza Baba Mtakatifu, na hiyo ianzie katika uwekezaji wakitazama familia,
elimu na kuwawezesha maendeleo na amani ya jumuiya nzima ya raia.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |