2017-10-11 16:08:00

Papa:Kila siku ni ukurasa mweupe wa kuandika matendo mema ya Mungu


Leo nataka kusimamia juu ya ukubwa wa matumaini ambao ni kuwa tayari na subira. Mada ya subira ni mojawapo  ya mwongozo wa Agano Jipya. Katika mahubiri ya Yesu kwa wafuasi wake aliwambia muwe tayari mmejifunga mikanda kiunoni  na taa zenu ziwe zinawaka muwe kama watumishi wanao mngojea Bwana wao arudi kutoka harusini ili wamfungulie mara atakapo bisha » (Lc 12,35-36). Ni maneno ya tafakari ya Baba Mtakatifu Francisko wakati wa katekesi yake ya Jumatano 11 Oktoba 2017 katika viwanja vya Mtakatifu Petro akiendelea na mfululizo  wa tafakari za matumaini ya Kikristo. Baba Mtakatifu anasema, katika kipindi baada ya ufufuko wa Yesu ni hali inayoendelea wakati mwingine ya matukio ya  faraha na uchungu  lakini wakristo wasijisahau kamwe. Injili inasisitiza kuwa, wawe kama watumishi wasio lala usingizi mpaka atakapofika Bwana wao. Na hiyo inadhihirisha ni  jinsi gani ya mkristo anapaswa kuwajibika na  jisni gani ya kutimiza hayo katika maisha yetu yote.

Yesu anataka maisha yetu yote yawe ya kuwajibika bila kuchoka na kutoa  shukrani kwa maajabu yake tunayo pokea kila siku. Kila asubuhi ni ukurasa mpya mweupe ambao mkristo analazimika kuandika matendo mema. Sisi tumekombolewa tayari na Yesu, lakini sasa tunasubiri ukamilifu wa maonesho hayo ya ukuu wake mahali ambapo Mungu atakuwa  ni wa watu wote na kila kitu. Lakini kakuna mwenye uhakika wa siku hiyo katika imani ya mkristo, Baba Mtakatifu anasisitiza,  siku ya Bwana atakapokuja hakuna hajuaye , lakini siku hiyo takapokuja  wakristo wote wawe tayari kupokea ukombozi ambao tayari unawafikia. 

Baba Mtakatifu ameuliza swali kwa wote walio udhuria katekesi hiyo katika viwanji vya Mtakatifu Petro, iwapo wako tayari kukutana na Yesu atakapokuja. Lakini siku hiyo itakuwa  ni ya furaha kubwa na kukumbatiwa kwa furaha , hiyo  ndiyo kukutana na Bwana, ni lazima kuishi kwa subira ya kukutana.
Akifafanua na kutoa mfano Baba Mtaktifu anasema, mkristo hakuumbwa kuwa mvivu au kukosa uvumilivu . Japokuwa anatambua kuwa uvuvi unaojitokeza wakati mwingine una manufaa na umejifunika katika fumbo la neema. Kuna watu ambao  wanavumilia kwa upendo  ba daaye  hugeuka kuwa kisima cha kumwagilia jangwa. Hakuna chochote kitokachopotea , hakuna hali ambayo mkristo anakumbana nayo na  isiwe na upendo mkamilifu. Hakuna usiku mrefu wa kufanya usahahu furaha ya machweo. 

Kadiri inavyozidi kuwa usiku wa giza nene ndipo likaribia kuchomoza jua.Iwapo tunabaki tumengana na Yesu hasa katika ubaridi  wa kipindi kigumu tusiwe kiwete, hata kama ulimwengu utatangaza kupambana dhidi ya matumaini,  hata wakisema  wakati ujao utakuwa ni mawingi meusi , mkristo anatambua vema kuwa wakati ujao  yupo Kristo atakayerudi tena. Je ni lini itatokea , hakuna anayejua, siku wala saa, lakini mwisho wa historia ya maisha yetu yupo Yesu wa huruma, inatosha kuwa na matumaini na siyo kulaani maisha. Kila kitu kitakombolewa anasema Baba Mtakatifu.
Yote upata mateso anaendelea, kutakuwa na kipindi cha kukasirika na ghadhabu, lakini cha muhimu ni kukumbuka kuwa  Kristo atafukuza vishawishi  vya kufikiria na  juu hisia za kukosea maisha.  Hiyo ni baada ya kumtambua kristo na  kufikiria historia ya imani na matumaini. Yesu ni kama nyumba ambayo sisi  tumo ndani yake na  madirisha yake ndipo tunatazama ulimwengu kwa nje . Kwa njia hiyo hatuwezi kujifungia ndani sisi wenyewe , hakuna kulia kwa uchungu kwa yale yaliyopita. Ni kutamani daima kwenda mbele na maisha endelevu ambayo hayatengenezwi kwa mikono yetu zaidi ni  Mungu mwenyewe anayehangaikia watu wake . Baba Mtakatifu ansisitiza, kila kitu katika giza kitakuwa na mwanga!

Ni lazima kufukiria kuwa Mungu hajidanganyi mwenyewe . Kamwe hadanyi! Mapenzi yake kwa ajili yetu hayana mawingu meusi, bali analinda na kuokoa moja kwa moja, kama asemavyo Mtakatifu Paulo kuwa, Mungu anataka  watu wote waokolewe na  wapate kujua ukweli (1Tm2,4). Kwa njia hiyo hatuna haja ya kujiingiza  katika matukio yenye ugumu , utafikiri  ni kama historia ya treni iliyopotea usikuni wake. Kukata tamaa siyo fadhila ya kikristo. Na pia siyo Ukristo wa  tabia ya kugeuza mabega, kwa maana kila mkristo lazima awe jasiri na kujihatarisha kwa ajili ya wema wa  wote, kama vile Yesu ambaye alitupatia wema huo na kuwa tunu msingi wa maisha yetu.

Kila siku katika maisha yetu , turudie kuomba kama wafuasi wake wa  kwanza kwa lugha ya kiaramaiko waliosema ”Maranatha" maana yake, "Uje  Bwana Yesu" (Rej: Uf 22,20)  Ni kiitikio cha wakristo wa kila muhongo na katika   ulimwengu wetu wetu wenye kuwa na mahitaji ya huruma ya Yesu .Katika sala zetu wakati wa kipindi kigumu tuweze kusikia sauti inayojibu Tazama mimi naja upesi  (Rej: Uf 22,7).

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.