2017-10-10 16:03:00

Mons. Vigano':Historia ya Nabii Yona ni kama historia ya kila mmoja


Mahubiri ya Monsinyo Dario Vigano' Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Mawasiliano Vaitican kwa washiriki wa Kozi ya Mafunzo ya Mawasiliano huko Orvieto Italia  yenye kauli mbiu "utawalwa: huduma kwa ajili ya wote" , tarehe 10 Oktoba 2017. Akitafakari somo la siku anasema, wameunganika kwa pamoja na furaha ili kustaajabia upendo wa Mungu alionao na kuendelea kutimiza ile historia ya binadamu  katika maisha ya kila mmoja. Somo la siku linahusu  historia ya Yona. Monsinyo anasema, Nabii Yona  ni historia ya uinjilishaji. Ni Nabii mtiifu aliyetumwa kwenda kuwatangazia watu habari mjema ya kuongoka kabla ya hasira ya Mungu haijangukia kwa watu wa Ninawi kutokana na dhambi nyingi zilizotendeka, japokuwa Mungu anawavumilia kwa unyeyekevu na pia kuwatumia mtu wa kuweza kuwapa tahadhali. 

Monsinyo Vigano anasema, kama asemavyo Baba Mtakatifu Francisko kuwa, Mungu hakuweza kuwatupa watu wake,  hawaachi washindwe na dhambi  kwa maana yeye ni mwaminifu na neema zake ni kubwa zaidi ya dhambi. Hilo ni fundisho la kujifunza kwa sababu tunavyo vichwa vigumu na hatutaki kujifunza. Lakini Mungu ni mkubwa zaidi ya dhambi, ana uwezo wa kushinda dhambi hata kubwa, za aibu, hata zile ambazo ni vigumu kuelezeka . Mungu anashinda dhambi hizo kwa njia ya upendo.

Hiyo ina maana ya kwamba Mungu anatawala na ndiyo maneno ya imani kwa Bwana ambaye katika uwezo wake, anajinyenyekeza na kuinamia binadamu Mungu anainama kutoa huruma na uhuru wa binadamu ambaye ameumbwa kwa mfano wake. Hiyo ni kwasababu tunapoondolewa dhambi, tunakuwa wazuri na kuwa mfano wa Mungu hakika (Rej. Hotuba Baba Mt. 14 Desemba 2016).
Upendo wa Mungu unasamehe yote hasa anakutana na moyo wa binadamu ulio tayari funguka kwa ajili ya kupokea neema na kutubu dhambi alizotenda. Na ndiyo historia ya mji wa Ninawi, na ndiyo  historia ya kila mmoja ambaye yuko tayari kujiachia  ili akumbatiwe na ukarimu, huruma ya Baba mwema na mwenye upendo mkubwa.

Hiyo ndiyo shule ya maisha ili upendo ulitolewa na Baba kwa njia ya mwanae, uweze kuwa  na maana katika kuishi kila siku, hasa kwa mantiki ya msamaha wa kweli na siyo kilipiza visazi, kukaribisha na siyo  kukatalia , kuwa na huruma na siyo kuwa na ugumu wa mioyo.
Monsinyo vigano aidha  anasema, neno ambalo limesikika liweze kuwa mwanga na ulazimwa wa kutambua mabaya , kukataa ubaya huo na kutazama yaliyo mema na kukaribisha. Kwa kufanya hivyo siku moja wote wanaweza kuimba kila siku zaburi “Sikiliza kwa makini sauti ya kilio changu (Zab129,1-2) 
Aktafakari juu ya Injili ya siku kutoka kwa Mt Luka, inaelezea juu ya Yesu na dada  wawili Marta na Maria. Monsinyo Vigano’ amesisitiza juu ya kutambua uwajibikaji katika shughuli za kawaida na maisha ya kiroho.

Katika shughuli za kila siku, ni muhimu kukumbuka neno la Mungu kwa maana pamoja na shughuli hizo, Yesu hajakataa , bali mi muhimu kuzingatia jambo lenye kuleta maana hasa katika usikivu wa neno la Mungu. Kwa njia hiyo katika maisha yetu ya kila siku yawe ni kukaa na familia, kazini au marafiki ni muhimu kukumbuka kusikiliza Neno.  Bila kufanya hivyo Monsinyo Vigano’ anasema, ipo hatari ya kuangukia kufanya kazi na kusahau roho ikakauka, mwisho wake ni kusahau yale mambo muhimu ya maisha ambayo yanakufanya uweze kuishi na kukabiliana na chamoto za kila siku.
Sr Angela  Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.