2017-09-29 16:56:00

Papa: Wito wa Malaika na sisi ni sawa,kushirikiana mpango wa ukombozi


Wito wa Malaika na sisi ni sawa, kwa kushirikiana pamoja katika mpango wa ukombozi wa Mungu, na hiyo imeandikwa katika maombi ya siku ya leo . Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri yake kwenye Kanisa la Mtakatifu Marta wakati wa tukio la Sikukuu ya Watakatifu Malaika Wakuu Michaeli, Rafaeli ina Gabrieli. 
Baba Mtakatifu Francisko anasema, tunaweza kusema kuwa sisi ni ndugu katika vito. Wao wako mbele ya Bwana  wakitoa hudima , wakisisifu na kutakafari utukufu wa Bwana na hivyo Malaika ni wakubwa katika kutafakari.Hata hivyo Bwana anawatuma kutusindikia katika safari yetu ya maisha.
Baba Mtakatifu akilezea uwajibu wa kila malaika anasema, Malaika wakuu watatu wanao wajibu wao katika safari yetu ya wokovu kwa mfano  Malaika Michaeli anapambana katika vita na shetani, ambaye ni joka kuu la kizamani ambalo linasumbua daima maisha yetu, linakaa ardhi hii kama lilvyo mdanganya mdanganya mama yetu Eva na baada ya kuanguka likamuhukumu mbele ya Mungu.
Kwa kutumia maneno ya ulaghai, kula tunda kwa maana utatambua mema na mabaya na mambo mengi. Yeye ni mdanyanyifu , kwa maana  shetani anatumia ulaghai  na ndiyo maana anasema mdhambi ni wangu.  Anatumia ulaghai, lakini Mungu anamtuma  Malaika Michaeli kupambana naye katikavita. Bwana alimwomba afanye vita na shetani huyo kwa ajili yetu sisi tuliyo katika safari kuelekea mbinguni. Malaika Mikaeli anatusaidia kupambana katika vita na hatuachi kwamwe tuingie katika ulaghai.
Malaika Michaeli anayo kazi ya kulinda Kanisa na kila mmoja, tofauti na kazi ya Malaika Gabrieli  ambaye ni mpeleka habari njema. Yeye alipeleka habari njema na ya wokovu  Kwa Maria, Zakaria na Yosefu. Hata Malaika Gabrieli daima yuko nasi , anathibitisha Baba Mtakatifu, anatusaidia katika safari yetu na hasa tunaposahau Injili  ambayo  ni Yeu amekuja  kwa ajili ya kutukomboa.
Malaika wa tatu, Baba Mtakatifu anaeleza, Rafaeli, ambaye anatembea na sisi na ili tusielekee  katika njia potofu. Kwa njia hiyo wasindikizaji  wetu katika  huduma ya Mungu na maisha yetu , wanatufundisha leo hii kusali kwa njia rahisi, kama vile , Michaeli atufundishe  kupamba na  kila mmoja atambue namna ya kupamba na maisha yake kuondokana na ubaya  wa shetani mwovu. Malaika Gabarieli atusaidie kupeleka habari njema ya wokovu kwa kuwatangazia wote kuwa yeye anaishi na tupo pamoja naye katika safari ya kuelekea kwa Baba yake.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya  Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.