Mkutano wa toleo la 69 la Gran Prix Italia, ambao ni Mkutano wa Kimataifa kuhusiana
na vipindi vya Radio, Televisheni na Inteneti ya kisasa katika utamaduni na usanii.
Tukio hili litafanyika huko Milano kuanzia tarehe 28 Septemba hadi 1 Oktoba 2017.
Nchi 31 kutoka mabara matano ya dunia hii wanashiriki ambapo kauli mbiu ya mkutano
huo inasema Uandishi wa habari katika kipindi cha habari za bandia. (Fake News). Kizingiti
cha radio”.
Katika tukio hilo, naye Monsinyo Dario Vigano Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Mawasiliano
Vatican tarehe 28 Septemba 2017 ametoa hotuba akisema, suala la uhandishi wa habari
katika kipindi cha Fake news unazungukia msingi mmoja tu ambao ni kuhakikisha vyanzo
vya habari juu.
Ni njia ya kizamani ambayo iliendelea kukua kwa nyakati na ambayo lazima kujikita kwa upya kuitafuta na kuinendeleza ili iweze kuwa kiini katika mawasiliano ya kisasa. Ni vema kumbuka na kuhakikisaha vyanzo vya vinavyojenga na kuongoza msingi wa uhandishi wa habari. Monsinyo Vigano anaendelea, habari za bandia leo hii ni changamoto kubwa ki ukweli inatoa mshituko wa habari, maoni na matendo yasiyo na maana na uhakika. Na katika mfumo wa mawasiliano ya kisasa, ukweli uko hatarini maana unegeuzwa kuweka nafasi ya pili katika habari.
Lakini hata hivyo anasema kwa upande mwingine hiyo imesababishwa na kwa mabadiliko ya kiteknolojia ambapo inakuwa vigumu kutumia makundi ya dhana ya zamani. Lakini wakati huo huo mazingira ya mawasiliano ya kisasa yana majukumu katika mtandao na vyombo vya Habari vya kijamii hasa mbele ya wasikilizaji wapya, wanaotumia simu, kwa maana tunaendelea leo hii kona jinsi gani kuna upungufu wa mipaka ya vyombo vya habari ambavyo tumezoea kufikia hadi sasa.
Huo ndiyo ufalme wa vyombo vya habari vinavyopishana , au vyombo vya habari vya kioevu, ambapo habari za bandia pia zinaendeshwa. Pamoja na habari bandia, na labda zaidi ya habari ya bandia, bado kuna mwenendo wa jumla. Na huo ni katika uwanja wa habari ambao kwa umma unaendelea kupoteza imani katika vyombo vya habari vya jadi.
Monsinyo Vigano anaonesha baadhi ya tafiti nchini Italia kuwa, kwa mujibu ya baadhi ya uchunguzi na tafiti inaonesha kuongezeka idadi ya Waitaliani wana dai kuwa na matumaini ya uwezo na ujasiri wa mtandao wa kuripoti kikamilifu , kwa usahihi, licha ya kuingizwa kwa habari za uongo kwenye mtandao ni asilimia 62% kati ya asilimia 49% ya vyombo vya habari vya jadi kulingana na utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Chuo Kikuu cha Urbino nchini Italia. Aidha Chuo hicho kinaongeza: chini ya moja kati ya washiriki 10 wanaamini kikamilifu katika vyombo vya jadi.
Kwa mfano, mwandishi wa habari, kwa mujibu wa maandishi pekee yanayoidhinishwa na Amri ya Januari 2016 ambayo imekusanya sheria zote juu ya mada hiyo, ina sahihi katika marekebisho na heshima ya vyanzo hasa, kwa misingi ya Kifungu cha 9, kwamba mwandishi wa habari: a) hurekebisha hata kwa kutokuwepo kwa ombi maalum, kwa haraka na kwa usahihi taarifa ambayo baada ya usambazaji haikuwa sahihi au isiyo sahihi; b) hatoi ripoti yoyote ambayo inaweza kuharibu sifa na utu wa mtu bila kutoa fursa za kurudia. Ikiwa hii imethibitishwa kuwa haiwezekani, awajulishe umma; c)kuthibitisha, kabla ya kuchapisha na kutoa habari za taarifa ya udhamini ambayo mtu anayehusika .Ikiwa haiwezekani inajulisha umma; d) huchunguza habari zilizopatikana ili kuthibitisha uaminifu wake;
e) huheshimu siri za kitaaluma na kutoa taarifa ya ikiwa vyanzo vinaomba kubaki
na siri; katika matukio mengine yote daima hutaja na wajibu huu huendelea hata wakati
wa kutumia vifaa, maandiko, picha, sauti ya mashirika na vyombo vya habari vingine
au mitandao ya kijamii; f) hakubali kulazimishwa au hali yoyote ya kutoa au kufuta
habari; g) haondoi ukweli wowote, maagizo au maelezo muhimu wa ujenzi wa habari kamili
wa tukio.
Monsinyo Vigano anabainisha kuwa, kanuni hizi za kale zinapaswa kukumbushwa na imani
kwamba inatoa usambazaji mpana wa vyanzo.
Mchakato wa utaratibu lazima ueleweke kama mazoea mazuri ya kuhakikisha habari sahihi, ubora zaidi, na juu ya yote kuheshimu katika mazingira ya mchakato wa uhusiano. Hali kadhalika anasema, inafaa kwa waandishi wa vyombo vya habari vya jadi pamoja na mameneja wa vyombo vya habari, watengenezaji video, wapiga picha, na takwimu nyingine zote za kitaaluma zilizohusika kila siku katika uzalishaji wa vyombo vya habari kwa njia mbalimbali.
Akielezea msingi wa Radio Monsinyo Vigano anasema, Redio ina uwezo mkubwa wa uzalishaji inatosha tu kwenda katika kipaza sauti au simu ili kuweza kwenda katika teknolojia ya mawimbi ya hewa. Haitajiki vifaa vingine vyenye utata au hasa vizito vinavyopaswa kuanzishwa ili kuingia kati yake. Kwa manano rahisi anasema radio inajihusisha katika kusembaza maelezo na habari ya haraka ambayo yana thamani kubwa na ya msingi.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |