2017-09-08 15:45:00

Msamaha unahukumu maovu na kuongoza njia ya uponyaji wa majeraha


Hotuba ya Askofu Mkuu Bernardito  Auza Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Ofisi za Umoja wa Mataifa New York  kwenye Kikao  kuhusu Utamaduni wa Amani tarehe 7 Septemba 2017. Askofu Mkuu ameanza na shukrani  kwa kupata fursa hiyo  ili kubadilishana mawazo juu ya kukuza Utamaduni wa Amani hasa kuhusiana na maendeleo ya watoto. Askofu Mkuu Auza anasema kuhusu mada ya watoto na utamaduni wa Amani, kwa upande wa Vatican wanaona kwamba bado haijaweza kufikia wakati mzuri , kwa sababu hivi Karibuni Kanisa Katoliki limeadhimisha miaka mia moja ya kutokea Mama Maria wa Fatima huko Ureno.

Sauti kuu kuhusu  umwagaji damu wa Vita ya kwanza ya dunia, ujumbe wa Fatima ulikuwa unaelezea juu ya Amani na ulikabidhiwa kwa watoto watatu ambao walikuwa na umri wa miaka saba,tisa na kumi.Ujumbe huu wa Amani ni muhimu hata leo hii kama vile miaka mia moja iliyopita. Vinasikika  hata leo vilio katika dunia nzima  mahali ambapo zinasikika  sauti za vita vya dunia kupigania Amani. Ni kama Baba Mtakatifu Francisko alivyosema kuwa mahali ambapo kuna migogoro  ya vurugu, vitendo vya ugaidi, ikiukwaji wa haki za msingi wa binadamu,na umaskini unaokithiri hunakwamisha juhudi za Amani.
Kukuza utamaduni wa amani kati ya watoto ni jambo muhimu kwa ajili ya Amani endelevu. Umuhimu wa kuhamasisha thamani hii kwa watoto ni kuwaelimisha katika utamaduni wa kukutana na ambao unahusisha  hali halisi ya heshima , kisikiliza kwa makini na ushirikiano bila haja ya kuvuruga au kupunguza utambulisho na hadhi ya mtu. Utamaduni huo utawawezesha watoto kijibu kikamilishi na kwa ufanisi katika kukabiliana na aina nyingi za vurugu, umaskini, unyonyaji, ubaguzi na aina aina nyingine zinazokumbwa mwanadamu.

Askofu Mkuu Auza anabainisha, kwa  njia hiyo Taasisi za elimu lazima kuwapa watoto mafunzo ya maana ya  sarufi ya majadiliano ambayo kama Baba Mtakatifu Francisko anavyothibitisha hivi karibuni kuwa  ni msingi wa kukutana na kuwapa  maana ya njia ya kuunganisha tamaduni na tofauti wa kidini. Kuimarisha vijana na watoto katika masomo ya sarufi hii  ya kiakili  katika mazungumzo  na kwa lengo la kugundua ukweli pamoja , utawaacha wakiwa na sababu ya kusisistiza  kujenga madaraja na kupata ufumbuzi wa kutafuta Amani dhidi ya aina mbalimbali zinazoleta  vurugu za wakati wetu.
Askofu Mkuu auza anasema Vatican inaamini kuwa hali ya kwanza katika kukuza utamaduni wa amani ni ulinzi na kukuza maono kamili ya mtu na utu wa kibinadamu. Kupunguza maono  ya binadamu hufungua njia ya kuenea kwa udhalimu, ukosefu wa haki , ukosefu wa usawa kijamii na rushwa. Utamaduni wa amani inamaanisha kupambana na udhalimu na kuong’oa mizizi yake nje, Kufundisha njia isiyo ya ukatili kwasababu ukosefu wa maelewano na ugomvi unasababisha vita. Amani inahusisha kukataa vurugu katika kuthibitisha haki za mtu. Kukabiliana na vurugu kwa kutumia vurugu kunaongeza  Vifo na uharibifu zaidi. 

Katika suala hili, kuimarisha utamaduni wa amani unajumuisha jitihada za kudumu dhidi ya silaha na kupunguzwa kwa kutegemea silaha katika uendeshaji wa masuala ya kimataifa. Kila juhudi katika mwelekeo huu, hata hivyo ukiwa ni wa kawaidia husaidia kujenga utamaduni wa amani.
Vatican inaendelea kutoa wito wa kuongeza nguvu zaidi katika kusisitiza uhusiano mkubwa kati ya kukuza utamaduni wa amani na kuimarisha jitihada za ukomeshaji wa silaha  na kuenea kwake. Kuenea kwa silaha hizo  huongeza wazi hali ya migogoro na matokeo yake ni  gharama kubwa za binadamu na ambazo hudhoofisha maendeleo na utafutaji wa amani ya kudumu.

Akifafanua zaidi juu ya hilo anasema,utamaduni wa amani unaweza kustawi tu katika utamaduni wa msamaha. Msamaha ni muhimu kwa upatanisho na kujenga amani, kwa sababu unafanya uponyaji na upyaji wa mahusiano ya binadamu iwezekanavyo. Kusamehe siyo  kinyume na haki lakini badala yake ni kutimiza, hivyo msamaha unahukumu maovu kwa maovu na kuongoza njia ya uponyaji mkubwa wa majareha yanayotokea ndani ya mioyo ya kibinadamu. Kwa hiyo, utamaduni wa amani unahusisha uamuzi wa ujasiri wa kuruhusu majeraha ya siku za nyuma utoweke  ndani kwa sasa na baadaye. Katika Ujumbe wake wa Siku ya Amani Duniani tarehe mosi Januari mwaka huu, Baba Mtakatifu Francisko anathibitisha kwamba amani ni zawadi, ni changamoto na kujitoa. Ni zawadi, kwa sababu inatoka katika moyo wa Mungu. Ni changamoto kwa sababu ni vema kwani ni ambayo haiwezi kamwe kuchukuliwa kwa lazima lakini inapaswa kupatikana daima. Na ni  kujitoa kwa sababu inahitaji juhudi ya dhati kwa watu wote kwa lengo la kuitafuta na kuijenga Amani hiyo.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.