2017-09-05 15:36:00

Papa amezungumza na Chama cha Shalom na kuwataka watoe ushuhuda wa kweli


Kushuhudia huruma ya Mungu na kuondokana na ubinafsi  wa kujitosheleza  mwenyewe. Ni moja ya maneno ya moja kwa moja katika lugaha ya Kihispania ya  Baba Mtakatifu Francisko alipokutana na Jumuiya chama Katoliki cha Kitume Shalom tarehe 4 Septemba 2017, ambapo wanachama wake wamepokelewa na kuongea na Baba Mtakatifu katika ukumbi wa Mwenye heri Paulo wa VI mjini Vatican.
Mazungumzo wakati mwingine yaliyo kuwa yenye matani mengi, lakini yaliyo jaa utajiri mkubwa na mawazo halisi ya maisha ya vijana wakati huo  washiriki walikuwa ni 4000. Kabla ya hotuba yake ya moja kwa moja na wazi, kwanza kulikuwapo na ushuhuda wa uzoefu wa baadhi ya wanachama wa Shalom na ambayo Baba Mtakatifu aliwajibu kwa lugha rahisi na wazi.

Baba Mtakatifu amesema, majibu aliyo yatoa ya jumuiya Katoliki ya Shalom iliyoanzishwa miaka 35 iliyopita, zaidi ni wito wa kushuhudi huruma. Ninyi hamwezi kuongea juu ya huruma badala yake ni kushuhudia, kushirikishana, kufundisha kuondokana na ubinafsi. Ni lazima kutangaza kwamba Mungu ni mwema ambaye anasubiri watu hata katika kipindi  kigumu cha maisha.Papa  anatoa mfano kuhusiana na hilo katika mfano wa mtoto mpotevu ambaye anasema kuwa baba yake alimsubiri, alipomwona kwa mbali alimwonesha nini maana ya huruma. Kutokana na hilo Papa amewaonya vijana ambao wanapenda kujitosheleza wao wenyewe, kuwa wabinafsi, kujifikiria wao weyewe na kwamba  katika utamaduni tunamoishi, umejaa ubinafsi, ambapoanasema ni  dozi ya kujipendelea, kujifikiria binafsi, kuwabeza wengine au kudharau wengine.

Hiyo ni hali ya kutoa  huzuni kwasababau ni kuishi kwa mahangaiko ya kupamba na  roho ya ubinafsi kila siku kwa sababu ya kutaka  kuonekana bora au mwenyewe na kumbe siyo hivyo. Kwa njia hiyo usijitazame katika kioo ambacho kinadanganya, badala yake watazame wengine. Baba Mtakatifu amewapa ushauri kwamba kila siku wanapojiangalia katika kioo bora kujifunza  kujicheka wenyewe, kwani katika utambuzi wa kucheka mwenyewe, inaweza kuleta furaha na kuona kishawishi  cha kuwaambukiza hata wengine badala ya kujipendelea binafsi.

Halikadhalika Baba Mtakatifu amegusia  pia suala la madawa ya kulevya , kutokana na kijana aliyetoa ushuhuda wa kuondokana na janga hilo.  Anasema, madawa ya kulevya ni moja ya zana ambayo imo duniani  tunamoishi na  inazaidi kutawala  na inazidi kutanda mizizi katika familia za leo, zilizopita, hata katika upendo na katika yote.Kilio cha Baba Mtakatifu ni kuona kwamba, kuishi katika dunia bila mizizi, hiyo ndiyo janga la madawa ya kulevya naili kuweza  kuondokana na madawa ya kulevya ni njia mojawapo ya utambuzi wa hakika  kwamba inawezekana kabisa kutengeneza mambo mapya na mema.
Katika kuelezea juu ya hili, amekumbusha juu ya safari ya Sinoni ya Vijana  ambapo amesema,wote ni lazima kuwa na mang’amuzi ya wito kwa ajili ya kutazana nini Bwana anataka katika safari ya utume, yaani kujitoa bila kubakiza kile  ambacho tumepokea bure. Huo ndiyo wito wa nguvu ambao ameutoa kwasababu anasema kutoa bure ni kujaza roho.

Tafakari la mwisho lilikuwa linahusu mtu mwenye umri mkubwa kwa maana ya uzee katika Jumuiya ya Shalom , amewasisitizia juu ya mazungumzo kati yao na vijana, kwamba ndiyo moja ya changamoto za ulomwengu huu. Vijana kwa thati wanahitaji kusikiliza wazee, kama pia ilivyo kwa wazee  kuwasikiliza vijana. Onyo lake Baba Mtakatifu anasema, wazee hawapaswi kuwekwa kabatini kama nguo zilizokunjwa na kuhifadhiwa ndani yake.
Ametoa mfano huo, kutokana na uzoefu wake alio ufanya hapo zamani kwamba, alikwenda na kikundi cha vijana katika nyumba ya wazee, vijana hao walipiga vyombo vya muziki na kutumbuiza, baada ye walianza mazungumzo, ambayo yalikuwa kati ya bibi na wazee ambayo  yalikuwa ya hekima.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.