2017-08-14 13:24:00

Colombia: wanawake watafanya maandamano ya kupinga unyanyaswaji


Ijumaa tarehe 8 Septemba 2017 wanawake karibia elfu tano wote wakiwa wanatazamiwa kuvaa nguo za rangi ya machungwa  wanatarajia kumpokea Baba Mtakatifu Francisko huko Villavicencio wakati wa Ziara yake ya kitume nchini Colombia, kwa ajili ya kuonesha wazi kampeni ya kupambana na unyanyasaji dhidi ya wanawake. Ni mashirika 30 ya vyama vya wanawake wa nchi walioanzisha mpango huo kama unavyoonesha katika Tovuti ya Kanisa la Colombia kati ya  matukio ya Ziara ya Baba Mtakatifu Francisko. Wametengeza tangazo linaoonesha kauli mbiu yao  isemayo “sisi wanawake wa Villavicencio,na katika dunia tunapiga hatua mbele kwa ajili ya kutaka uhuru wa maisha dhidi unyanyaswaji”.

Mwakilishi wa chama cha“El Meta na mirada de Mujer”, Nancy Gómez Ramos, amefafanua  lengo la mpango wa kuanzisha suala hilo linalokwenda sambamba na ziara ya Baba Mtakatifu Francisko ya kwamba ni kutaka kumshirikisha katika mapambano dhidi ya unyanyasaji wa wanawake ambapo kutoka katika eneo la Villavincencio wanakuza heshima kwa ajili ya haki ya idadi ya wanawake mahalia na katika dunia kwa ujumla.
Hali kadhalika hata  mwakilishi wa Chama kingine  cha wanawake kiitwacho Comuna Tres cha Villavicencio, ameeleza ya kuwa, kwa njia ya vyama hivyo, wanachama wote wanayo matumaini ya kufungua uwanja mpana ndani ya ziara ya Baba Mtakatifu ili kuweza kuonesha wazi nafasi na wajibu wa wanawake katika mchakato wa kupunguza vurugu nchini Colombia.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.