2017-05-27 10:23:00

Huduma ya Afya siyo bidhaa,ni haki kwa wote, isiwe na upendeleo!


Afya siyo bidhaa ya kutumia,bali ni haki ya kila mtu na kwamba kupata huduma za afya isiwe kwa upendeleo, pamoja na majengo zenye nguvu na mifumo ya afya ni lazima kuweka kipaumbele cha maisha ya mwanadamu na mahitaji yake  kimwili, kidhamiri na kiroho,vilevile kupata matibabu katika kuheshimu zaidi utakatifu wa maisha ya binadamu katika hatua zake zote ikiwa ni pamoja na kutunza hadhi ya kila mtu. Ni baadhi ya mambo muhimu yenye nguvu juu ya  afya ya maisha ya binadamu katika hotuba iliyotolewa na Askofu Mkuu Ivan Jurkovič, Mwakilishi wa Kudumu wa Vatican Katika Umoja wa Mataifa kwenye Mkutano wa 70 wa dunia  kuhusu Afya ambao umeanza tarehe 22 hadi 27 Mei 2017 huko Geneva Uswiss.

Mwakilishi wa Vaticana anatambua uhamasishaji wa Afya ambao unahitaji kuheshimiwa na msingi wa mkataba wa agenda  2030 kuhusu maendeleo endelevu ambapo pia unawakilisha zaidi mambo muhimu kwa ajili ya kuimarisha uchumi jamii. Askofu Ivan  anabainisha kwamba mifumo ya afya inazidi kudorora, pia  kuwa kizingiti kikubwa katika nchi nyingi ,matokeo yake ni ukosefu wa bima na huduma msingi za afya. 
Changamoto za sasa na za haraka duniani anasisitiza;  ni kwa upande wa afya ambapo inatakiwa mifumo ya afya iliyo bora, yenye uwezo wa kutoa huduma inayofaa na inayopatikana kwa ajili ya kuzuia na kutibu wote, kwa namna ya pekee kwa watu wanye kuhitaji ,kama vile maskini  wanaoendelea kuongezeka katika jamii, waliobaguliwa, wahamiaji , wakimbizi ambao kwa sasa wanawakilisha katika jamii wasiwasi na ishara za nyakati hizi. Kwa mujibu  wa Askofu Mkuu Ivan anasema haitakiwi na hakina mtu wa kusahaulika.

Kama alivyoeleza Baba Mtakatifu Francisko kwamba kipimo na rahisi zaidi cha utendaji wa kuweza kufikia malengo ya agenda ya maendeleo endelevu iwapo  yataanza  kujikita katika vitendo mara moja , kwa watu wote  na  kwa ajili ya manufaa ya wote kiroho na kimwili inavyotakiwa . Mifumo ya afya yenye nguvu na kweli ni ufunguo wa kufikia melengo endelevu ambayo zaidi ni kuhakikisha maisha na afya na kukuza ustawi wa kila mtu na kwa kila rika la maisha ya binadamu. Juhudi zinazofanywa katika ngazi ya kitaifa kwa  kujenga mifumo ya afya bora kwa hakika zinahitaji mwendelezo wa uongozi kiufundi kutoka Shirika la Afya Duniani, pamoja na kuunga mkono na wadahu wa washirika ya maendeleo ili kuondokana na ukosefu wa rasilimali za kifedha katika sekta ya afya. Aidha, pamoja na miundombinu na  imara ya  kuaminika, mifumo ya afya ni lazima kuweka mbele utu wa binadamu na mahitaji yake kimwili, kidhamiri na kiroho, utoaji wa huduma bora katika kituo,kwa kuheshimu utakatifu wa maisha ya binadamu katika hatua zake zote na hadhi ya kila mtu.

Halikadhalika Askofu Mkuu Ivan anasema;  kama mataifa yatajizatiti katika kujenga , kuwekeza na kutekeleza hatua za kukuza maendeleo na miundo mbinu katika ujenzi wa mifumo ya afya inayotakiwa, ni muhimu kwamba, serikali wasizingatie utaratibu mmoja tu wa kusimamiwa na taasisi za serikali, bali wakumbuke kuwahusisha kuanzia wadau wakuu , hasa mashirika ya dini ambayo hutoa mchango  mkubwa katika  utoaji wa huduma za afya muhimu kwa watu . Aidha anathibitisha kwamba kwa dhati katika nchi nyingi, kuna mashirika mengi ya dini na taasisi nyingine za kidini na zisizo za kiserikali ambazo wanachukua wajibu muhimu kwa ajili ya mifumo ya afya na hivyo wanapaswa kujumuishwa katika uundaji wa sera za afya  kisias. Lazima  kuwa na upatikanaji wa rasilimali za kutosha ili kuhakikisha nguvu na uwezo wa shughuli hizo katika sekta ya kidini na mashirika yasiyo ya  kiserikali zinapatikana.

Askofu anaendelea kueleza ; Mifumo ya afya inayofanya kazi vizuri, ni lazima iwe na mambo mengine muhimu na hasa maji ya kuaminika, madawa na teknolojia. Hata hivyo, hali halisi, kama ilivyojitokeza katika ripoti ya  Sekretarieti  ya Umoja wa Mataifa kuhusu  maendeleo katika utekelezaji wa Ajenda ya Maendeleo 2030 ya Maendeleo Endelevu, kuhusiana na upatikanaji wa madawa muhimu ya kuchaguliwa, inahitaji hatua za maamuzi kwa upande wa jumuiya ya kimataifa.  Hiyo ni kwasababu imenukuliwa kwamba upatikanaji wa wastani wa madawa muhimu yaliyochaguliwa ni asilimia 56% tu katika sekta ya umma kwa nchi zenye kipato cha kati. Aidha bidhaa  mpya bado ziko mbali zaidi kufikia mahitaji ya afya ya watu wanaoishi katika nchi zinazoendelea.
Na kiasi cha asilimia 1% tu ya fedha zote kwa ajili ya utafiti na maendeleo ya afya ni lengo kwa ajili ya magonjwa yanayoathiri nchi zinazoendelea. Kwa njia hiyo Askofu anatoa ushauri kwamba, ni lazima kuanzisha ushirikiano ambao unawezesha kuwa na mwendelezo wa wa utafiti na maendeleo katika sekta ya afya ambayo ndiyo inahitajika na mahitaji ya ya afya yeyewe ,hatimaye kuhakikisha idadi kubwa ya dawa muhimu  inawafikia wote.

Askofu Mkuu Ivan anamalizia akisema; kama Papa Francisko alivyosisitiza kwamba ,"Afya, kiukweli, siyo  bidhaa, bali ni haki kwa watu wote na kwamba kupata huduma za afya isiwe kwa upendeleo . Kwa hali hiyo  Baraza jipya la Kipapa kwa ajili ya huduma ya mandeleo ya watu inaaandaa Mkutano wa Kimataifa kuhusu mada ya” kukabiliana na tofauti kimataifa katika afya", ambayo itafanyika katika mjini Vatican kuanzia tarehe  16-18, Novemba 2017. Askofu Mkuu anawaalika kwamba;kuushiriki kwao itakuwa ni mwafaka !

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.