2017-05-24 14:24:00

Waamini 15 nchini Ufilippini kutekwa nyara,na Kanisa moja India kuharibiwa


Maeneo ya Makundi ya Kiislam Maute yanayojitangaza kuwa na mahusiano na serikali ya Kiislam , walivamia Kanisa Kuu Katoliki la mji wa Marawi nchini Ufilippini na kuwateka nyara  waamini karibu 15 kati yao akiwemo Padri mmoja watawa na walei ambao walikuwa wanasali. Ni taarifa zilizothibitishwa na Askofu Mkuu  Edwin De la Pena  Mwakilishi wa Kitume katika Mji wa Marawi kwenye kisiwa cha Mindanao Kusini mwa nchi ya Ufilipini. Lilikuwa ni kundi karibu la magaidi 100 wa Maute walioshambulia mji huu ambapo Rais wa Ufilippini Bw. Rodrigo Durterte ameagiza mji kulindwa na sheria ya kijeshi katika kisiwa hivho.

Habari kutoka katika gazeti Katoliki la Fides zinasema, Askofu anasema kuwa tarehe 24 Mei 2017  ni sikukuu ya Mama Maria msaada wa Wakristo hivyo waamini walikuwa Kanisani wakisali siku ya mwisho ya Novena kabla ya sikukuu. Magaidi walingia kwa nguvu Kanisani na kuwateka nyara watu ambapo wamewapeleka sehemu isiyojulikana. Kwanza waliingilia nyumba ya Askofu  na kumteka nyara Katibu Msaidizi wa Askofu, Padri Teresito Soganub. Na baadaye kuchoma moto Kanisa Kuu ambalao limaharibika.

Magaidi hawa walishambulia mji na kuwaogopesha watu ambapo nyumba zimefungwa wakiwa wanasubiri wanajeshi anasema askofu. Aidha Askofu Mkuu anasema ili kutuliza nchi hii damu ni kama kwamba  itamwagika kwani kwa upande wa watekwa nyara hakuna habari yoyote ambayo imeshapatika, japokuwa mchakato umeanzishwa kati ya Kanisa na viongozi wa kiislam; ni matumaini ya kwamba mchakato unaweza kusaidia ili watu waliotekwa nyara waweze kurudi salama salimini. Anaongeza, kwa maombezi ya mama Maria msaada wa wakristo ndugu hawa wanaweza kupata msaada na kurudi.
Pamoja na haya mashabulizi ya magaidi , Rais wa nchi Duterte amehairisha ziara yake ya kwenda Moscow Urusi  ili kuwa karibu na watu wake wa ufilippini kukabiliana na kipeo hicho. Kikundi hicho cha magaidi kimesambaratika hadi kuchoma moto magereza ya wafungwa na mashule mawili ambapo sasa wanajeshi wamezingira mji wote. Mkuu wa Mkoa wa Marawi India  amewaomba wanajeshi wasitumie mabomu katika mji huo wanamoishi watu karibia raia  2000 zaidi wakiwa ni waislam.

Na nchini India  hata matukio mengine kama hayo  yametukia  katika jimbo Kuu la Hyderabad nchini humo na kaharibu Kanisa la Mtakatifu Mama Maria wa Fatima.
Ilikuwa ni siku ya Jumapili asubuhi 21 Mei 2017 kikundi cha watu kwa hasira karibia 100 waliingilia Kanisa lenye kupewa heshima ya Mama Maria wa Fatima  katika Kijiji cha Jimbo la Hyderabad. Washambuliaji hao waliharibu msalaba na kuvunja Sanamu ya Mama Maria wa Fatima. Kanisa hili lilikuwa jipya ambalo lilitabarukiwa tarehe 13 Mei 2017 mwaka huu kwa namna hiyo ni uchugu wa jumuiya nzima na Askofu Mkuu wa Hyderabad.
Kanisa hili lilitabarukiwa tarehe 13 Mei  2017 na Askofu Mkuu Thumma Bala, siku ambayo mama Kanisa Katoliki lilikuwa linaadhimisha miaka 100 tangu kutokea kwake  mama Maria wa Fatima.

Askofu anasema tendo la kuharibu sanamu ya mama Maria ni unajisi  na inatia uchungu na huzuni  kwa hisia za waamini wote wa jumuiya. Aidha Askofu Mkuu anasema,  baada ya upelelezi wa maafisa polisi, watafanya liturujia ya kusafisha. Masikitiko makubwa pia yamenoshwa na  Sajan K. George Rais wa Baraza la Makanisa ya Kikristo  nchini India (Global Council of Indian Christians).
Kwa mujibu wa polisi, shambulio hili inaweza kutokana na mgogoro wa ardhi iliyojengwa Kanisa jipya na kusababishwa wazalendo wenye itikadi kali kutopendelea ishara ya Kanisa hilo. Lakini pia hizi ni ishara za kuonesha jinsi gani Wakristo wanaendelea kuonewa pia kuwa na uvumulivu mkubwa katika nchi ya India.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.