2017-05-18 15:21:00

Ask.Auza:Manyanyaso kwa wanawake ni mazito yasiyoelezeka !


Wito wa nguvu kwa nchi zote za Jumuiya ya kimataifa ili waweze kutoa kipaumbele cha kupambana na unyanyasaji kijinsia na pia vurugu, ameutoa Askofu Mkuu Bernadito Auza Mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Baraza la Umoja wa Mataifa huko New York. Askofu Mkuu ametoa hotuba hiyo mapema wiki hii katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati wa majadiliano kuhusu mada ya “wanawake, amani na usalama”.
Askofu Mkuu anasema ,ni mateso makubwa na yasiyoelezeka kwa upande wa wanawake wanao endelea kuathirika kwa  ukatili wa kiajabu ambapo siyo rahisi kuweka moto huo chini ya miguu na  kufumba macho bila kuwa na msukumo wa kuinglia kati.

Kwa nguvu zote Askofu Mkuu Auza amehusisha juu ya ripoti ya mwisho iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa kuhusu unyanyasaji wa kijinsia na  katika vita. Amebainisha  kuwa hali hii inahitaji utelekelezaji wa haraka kwasababu ameorodhesha matukio hayo kuwa ni pamoja na utekaji nyara, husafirishaji wa watu, utumwa wa ngono, ukahaba , utoaji wa mimba ,ugumba wa kulazimisha na ndoa za kulazimisha.  Kwa mantiki  hiyo Askofu Mkuu Auza anasema ni tishio  na uhalifu mbaya usiolezeka  kwa kuzingatia matumizi ya unyanyasaji wa kijinsia kama mbinu za ugaidi.Uhalifu huu hasa wa matendo yaliyotajwa katika ripoti ni kama litania ya maovu.

Hiyo ni kwasababu inaonesha ni jinsi gani kuna haja ya  kuhamasisha dhidi ya  za magaidi ambao wanazdi kutishia  kugawanya watu, kulazimishwa watu  kubadili dini au  mabadiliko kwa njia ya ndoa ,kukandamiza haki msingi  za wanawake, magaidi kupata faida kwa njia ya biashara ya ngono ,magaidi kuwanyang’anya watoto ndani ya familia na kuwafanya wanyamaze , au kutoa wasichana  wawe wathirika katika kupigana kwenye vita kwa fidia, magaidi kuwatumia wanawake au wasichana  kama wanavyotaka pia kuwatumia wasichana kama ngao za binadamu  kwa manufaa yao kwenye mabomu ya kujitoa muhanga.

Kwa njia hiyo Askofu Mkuu anasema kuna  ushahidi mwingi wa kuthibitisha kwamba wanawake na wasichana ndiyo walengwa kama mbinu ya kujenga hofu ambayo huleta uharibifu kwa utashi wao na kuwafanya kama mashine  za  magaidi wanaopata kipato kwasababu ya kuwatumia.
Katika kukabiliana na majanga haya kwa utambuzi  huu wa vurugu na mateso  Askofu Mkuu mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika Baraza la Umoja wa Mataifa New York anamalizia akiwa na matumaini kwamba katika  ulimwengu wa wanawawake na wasichana ambao adhi yao imekiukwa, Baraza la Usalama wanaweza kuingilia kati na kwamba matumaini yake yasiwe ya bure.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.