2017-04-19 16:28:00

Timu ya michezo Vatican kwenda Ureno katika kushiriki mashindano


Timu ya wanamichezo wa Vatican (St Petr’s Cricket Club) iliyoazishwa Oktoba 2013 na Baraza la Kipapa la Utamaduni  litakwenda kupambana na timu michezo za umoja wa makanisa kwa ajili ya  mazungumzo ya kiekumeni  Ureno.
Timu  hii ilianzishwa kwa mawazo ya Balozi  wa Australia aliyeko katika  Ubalozini Vatican, John McCarthy kwa lengo la kujenga madaraja ya dini na utamaduni, kwa njia ya michezo. Katika timu ya Vatican washiriki wa timu hiyo ni  Mapdre, mashemasi na waseminari kutoka nchi ya India, Pakistan, na waingereza wanaosoma  katika vyuo mbalimbali vya kipapa Roma.

Mashindano ya mwaka  huu wameamua kwenda kuchezea  nchinii Ureno, kutokana na tukio la miaka 100 ya kutokea Mama Maria huko Fatima. Wachezaji watakabiliana na wanamichezo kutoka nchini Ureno  Hispania na Uingereza , wakiwa ni mchanganyiko wa dini tofauti , wakiwemo waislam , wayahudu na wahindu.Siku ya kwanza watazunguka na kutembelea Kanisa Kuu la Mama Maria wa  Fatima. Mashindano ya mchezo wa kwanza uli fanyika Septemba 2014 , kabla ya tukio hili kuanza safari kuelekea Uingereza, Baba Mtakatifu Francisko alikutana  katika mkutano binafsi tarehe 9 Septemba 2014.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahi ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.