2017-04-08 08:24:00

Inawezekana maendeleo endelevu katika sayari iwapo mgawanyo ni sawa!


Ni kuheshimu maisha kwa hali zozote na hasa kwa wale wadhaifu wasio kuwa na kuwa na mtetezi  , kwa mfano kuanzia hatua ya kutungwa kwa mimba,wazee, au walemavu, ni wito wa nguvu   uliotolewa na Askofu mkuu Bernadito Auza mwalikilishi wa Kudumu  wa Vatican katika Baraza la Umoja wa Mataifa  hivi karibuni katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa mjini New York , mkutano ukiwa unahusu juu ya maendeleo endelevu na ongezeko la watu.
Askofu Mkuu amesema, kwa miaka ya hivisasa kumekuwa mazungumzo kama vile bomu la ongezeko la watu ambalo limepelekea baadhi ya serikali kufuata siasa  kali ,zinazo unga mkono juu ya uchunguzi wa watu, wakitafuta njia rahisi lakini inayohatarisha rasilimali  na kutokuendelea kwa nchi  kama vile matumizi ya vidhibiti mimba kwa vizazi endelevu.

Askofu Mkuu anakubaliana nayo japokuwa anasisitiza ulazima wa kufikiria namna tofauti katika kubainisha kanda na taifa.Inabidi kutofautisha watu katika nchi zitakazo edelea kuongezeka watu kwa wakati  imfupi  na kwa upande mwingine ni lazima kutazama zile ambazo hakuna ongezeko lolote , karibu ni sufuri , na  wanafanya uzoefu kuona  upungufu wa idadi ya watu.Askofu Mkuu Auza amesema,kama ni kweli ya kwamba mgawanyo usio sawa wa watu na rasilimali unaleta kizingiti cha maendeleo endelevu  katika mazingira, inabidi pia kutambua kwamba ongezeko la watu ni sawasawa kabisa na kushirikisha kwa mali, katika jitihada za kuondoa umasikini, kutengeneza  ajira na kutunza mazingira.
Mitindo ya kisasa ya kuzuia mimba siyo jibu amesema Askofu Mkuu Auza. Anayasema hayo kutokana na kwamba nchi zinazoendelea idadi ya watu inapungua kwa kiasi kikubwa  kwa viwango vya kutisha,kutokana na  sababu mojawapo kubwa ya  matumizi ya vidhibiti vya mimba na sababu nyinginezo nyingi za kisasa wanazo taka ziwe hata katika nchi zinazoendelea.Kwa namna hiy askofu Mkuu anaongea kusema rasilimali za sayari hii zinatosha bali daima zinatumika kwa namna isivyotakiwa , na bila kuwa na mgawanyo mzuri.Kwasababu katika sehemu zilizoendelea , kuna hata matumizi makubwa , na wakati huo matumizi ni madogo katika  ngazi ya umasikini, vilevile ndiyo wahusika katika masoko kwani wanazuia nchi masikini kuingia katika masoko ya nchi tajiri, katika mgawanyiko wa rasilimali na katika uharibifu wa mazingira.

Katika nchi zinazoendelea, kinyume ni kwamba zinazidi kuongezeka ukosefu wa haki na umasikini ambao unasababishwa na rushwa ,vurugu za kivita , na maafa mengineya asili lakini yaliyosababishwa na binadamu ambaye uzuia kukua kwa afya njema ya watu.
Askofu Mkuu Auza anatoa ushauri katika kutoa jibu juu ya suala hili muhimu kuelekeza mambo matatu tatu, ya kwanza ikiwa ni mshikamano, amani na usalama. Hiyo inahitaji mabadiliko ya kisiasa, kikazi, kijamii, huduma, kwa pande zote mbili ikiwa katika nchi zilizoendelea na zile zinazoendelea.Inahitajika mkakati wa maendeleo endelevu yanayo mtazama mwanadamu na utu wake kwa ujumla,kuanzia wale walio baguliwa na kwa kuwashirikisha wote siyo katika  vigezo vya uzalishaji au kutokuzalisha, bali kuanzia na thamani ya kila mtu awe kijana au mzee.
Anaongeza akisema hakuna yoyote anayepaswa kuachwa nyumba kwasababu wote tunapaswa kushrikishana mizigo yetu.Lakini anaonya kwamba nchi masikini zisiendelee kutoa misaada ya masharti kwa ajili ya vidhibiti mimba.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.