2017-04-01 15:48:00

Ziara ya kitume ya Askofu Mkuu Hoser huko Medjugorje kuanza rasmi


Tunajikuta katika sehemu wamapokusanyika mahujaji wengu, tuombe wote kwa maombezi ya Mama wa Mungu, ili afungue mioyo yetu na akili zetu tuwe na neema za Mungu katika mafundisho ya Kanisa na Neno la Mungu. Kwa njia ya Roho Mtakatifu afungue maisha yetu na hata roho ya Kanisa ili tuutafute ukweli wa Mungu juu yetu na hata ukweli wa Mungu juu ya binadamu.
Ni maombi ya Askofu Mkuu Henry Hoser mjumbe maalumu wa Vatican, aliyotoa kwa waamini wote walio kusanyika pamoja katika parokia ya Mtakatifu Yakobo Medjugorje. Taarifa kutoka Shirika  la Habari la Sir linasema Askofu Mkuu wa Varsavia-Praga nchini Poland alifika tarehe 29 Machi 2017 mchana akiwa amesindikizwa na Padre Miljenko Šteko Mkuu wa ndugu  Wafranciskani Kanda ya Erzegovina, mara baada ya kupitia  nchi ya Sarajevona  Mostar.
Ikumbukwe hivi karibuni Baba Mtakatifu Francisko amemteua Kardinali Hoser Askofu Mkuu wa Varsavia Henryk Hoser nchini Poland kwenda huko Medjugorje kwa ajili ya ziara ya kutembelea na kuona maendeleo ya kichungaji kwa mahujaji wengi wanao fika kusali katika eneo hilo, na hivyo ziara yake imeanza rasmi.

Alipofika Medjugorje amepokelewa na Padre Marinko Šakota, paroko  wa  Medjugorje na wenzake ndugu kike na kiume wafranciskani wanao toa huduma katika parokia hiyo, hata  mahujaji. Wakati wa kutoa salam, amesema kuwa eneo hilo kwa sasa linajulikana ulimwengu mzima. Na kuongeza kusema,Baba Mtakatifu amejali kuendeleza matendo ya toba ya watu wanao elekea katika eneo hilo. Hii ni sehemu mojawapo ya utume na kuhakiki utume wa kichungaji katika eneo hilo kwa kutoa mwongozo kwaa ajili ya maelekezo endelevu ya kichungaji katika eneo hilo.
Aidha amemalizia akisema, nimekuja kutoka katika eneo lenye kuwa na ibada ya Mama wa Mungu Maria ni Malkia wa Poland, hivyo ni matashi mema ya kwamba nanyi mpate kufanya kama Mria Malkia katika maisha yake.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.