2017-03-18 15:26:00

Tarehe 23-27 Machi Makutano ya kukumbuka manyanyaso ya Wakristo


Shirika la Kipapa la kuhudumia Makanisa hitaji wameandaa makutano kuanzia tarehe 23 hadi 27 Machi 2017  katika miji mitatu ya Ufaransa na Monaco,makutano hayo yanaitwa “Usiku wa Mashuhuda”. 
Katika makutano hayo  watatoa ushuhuda Padre Jacques Mourad  kutoka nchi ya Syiria wa Jumuiya ya Mar Moussa ambaye  kwa miezi mitano alikuwa ametekwa nyara na inayojiita serikali ya kiislam, Padre Philippe Blot mmisonari mmoja wa Paris, anayejishughulisha  na wakimbizi  kutoka Korea ya Kaskazini, Mtawa Marie-Catherine Kingbo Mwanzilishi wa Shirika watawa wanawake la Watumishi wa Kristo huko Niger.Hawa watakuwa mashahidi wakuu watatu katika usiku shuhuda kwa mwaka 2017.

Pamoja  na shuhuda hizo kwa namna ya pekee katika Kanisa kuu ya Notre Dama kwenye  Mji Mkuu Paris ,Ijumaa 24 Mchana misa Takatifu itaadhimisha na Askofu msaidizi  Jérôme Beau .Baada ya maadhimisho itafuata mkesha. Makutano ya ushuhuda huo umefikia mara ya 9 tangu yaanzishwe, kwa lengo kutaka watu watambue hali ngumu  na manyanyaso yanayo endelea kuwakumba wakristo, katika kutafuta namna ya kuzuia na pia kurokuendela kunyamaza kuhusiana na matukio hayo.Taarifa zinasema watu watatu walio alikwa kutoa ushuhuda, wataongela zaidi juu ya shughuli zao za utume.
Pamoja na hayo watafanya maandamano ya sala wakiwa na picha za mapadre na watawa , walio uwawa miaka ya hivi karibuni kutoka nchi ya Mexco, Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na nchi nyinginezo duniani kote.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.