2017-03-15 14:25:00

DRC: Waseminari 25 kukombolewa na kurudi majumbani kwao


Waseminari 25 wameokolewa na Kikosi cha wanajeshi wa Kulinda amani cha  Umoja wa Mataifa nchi ya jamhuri ya Kideomkrasi aya Congo (DRC). Waseminari hao waliokolewa kutoka Mbuji-Mayi  kwa  njia ya helikopta , walikuwa moja ya kikundi kilichopotelea msituni baada ya mashambulizi ya seminari yao Kuu ya Malole huko Kananga Kasai ya Kati.Wanamgambo ni wafuasi wa Kiongozi marehemu Kamwina Nsaputarehe 18 Februari 2017.
Waseminari hao wamekombolewa baada ya wito uliotolewa  na Askofu Emmanuel Bernard Kasanda Mulenga ,askofu wa Jimbo la Mbuji-Mayi. Waseminari 25 wamerudi sasa katika familia zao baada ya kuzuiwa kukaa  Kananga kwasababu ya barabara inayo unganisha Mbuji -Mayi  kuzuiwa, kutokana na uwepo wa wanamgambo wa Kamwina Nsapu.

Ikumbukwe kwamba,  tarehe 18 Februari 2017 wanamgambo wafuasi wa Kamwina Nsapu walivamia Seminari kuu ya Malole Kananga ya  Kasai ya Kati katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo . Wanamgambo hao walivunja mitambo ya kulinda  seminari hiyo,walivunja milango yote na kuwaingilia. Waliharibu vyumba vyao na kila kitu kilichokuwa ndani, pia kuingilia vyumba vya walimu wao na kuchoma masanduku yao.Taarifa hizo zilitolewa kwa njia ya Radio Okapi na Gombera  wa Seminari hiyo Kuu Padre Richard Kitenge . Hata tarehe 18 Februari 2017 Baba Mtakatifu Francisko aliwakumbuka  watu hao wakati wa sala ya Malaika wa Bwana na kutoa masikitiko yake  juu ya uharibifu na nguvu wanao fanya  wanamgambo hao  wa kiongozi Kamwina Nsapu aliyeuwawa mwezi Agosti mwaka jana.Naye Askofu Félicien Mwanama Galumbulula alikuwa amelaani vitendo vya kutisha visivyoelezeka dhidi ya watu kutokana na wanamgambo hao.

Sr Angela Rwezaula

idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.