2017-03-14 15:02:00

Ndugu wadogo katikaTamasha la Muziki kwa ajili ya uinjilishaji


Kuunganisha ngoma, muziki katika tamasha ndiyo dhamira kubwa ya kuwafanya vijana wagundue furaha ya Injili.Ni lengo la baadhi ya ndugu wadogo wa Shirika la Mtakatifu Francisko wa Asisi ambao kwa miaka mingi wamejihusisha katika utume wa uinjilishaji,na  kujituma kuweka uhai kwa kuandaa tamasha lenye kauli mbiu “wewe ni mzuri na ndiyo maana uko duniani”. 
Hii ni sala katika muziki ,ni kipindi cha kufungua moyo wa matumaini na imani kwa Mungu,ni wakati wa kujisikia kitu kimoja, ni kukaa pamoja katika njia hiyo na kushukuru Mungu kwa  maisha uliyopewa:”Wewe ni mzuri kwa maana hiyo uko duniani”.Tamasha la uinjilishaji lilifikiriwa na kuanzishwa na ndugu wadogo wa wafranciskan, licha ya  kwamba mawazo yao hayo pia yamekubaliwa na  waimbaji na wanamuziki kama vile Andrea Vass na Luca Arosi, wote wamechangua kuongelea juu ya Injili moja kwa moja,hasa kwa kutumia lugha ya sasa ambayo inapendelewa na vijana , kwa kumia nyimbo maarufu ziwe kama zana kwa ajili ya kugundua uzuri wa kweli na wa kina.

Mwandishi wa Habari wa Radio Vatican alikutana na mmoja wa waanzilishi wa Tamasha hilo ndugu Mdogo  Matteo Della Torre  anaye ishi katika Jumuiya mojawapo ya Brescia nchini Italia na kusimulia juu ya mpango huo ulivyoanza.”Tumefikiria namna gani ya kuoanisha Habari Njema na lugha ya kisasa ambayo inaeleweka kwa haraka na vijana, kwa  kuweka pamoja ngoma na muziki , pamoja na mawazo yetu ya hayo ni pamoja na kufanya lugha iwe nzuri na mpya kwa vijana ambayo wanapendelea kuitumia , na katika kueneza maneno ya Mungu”
“Kwa njia hiyo tamasha la unjilishaji linageuka kuwa muda wa sala kwa kuishi katika mantiki ya ufunguo wa kileo ambapo vijana wanapenda kufanya uzoefu na hata kuanza kujiuliza na kujitafiti wao wenyewe kwa namna ya kina”.Anapngeza,”kwa hakika siyo kusema uzuri ni wa kushangaza tu kama tulivyozea kutazama na kusema bali, uzuri pia unapaswa kumelemeta,kwa upande wangu ni jambalo linaloleta maana zaidi”.

Tamasha la kwanza la uinjilishaji limefanyika huko Rezzato Wilaya ya Brescia Desemba mwaka jana .Vijana miambili waliweza kushiriki na  kuwa pamoja kwa kutafakari, kutokana na kwamba waliandaa tamasha hilo katika sehemu mbili ya kwanza ilikuwa inahus kutazama uzuri wa kisanii kwa namna hiyo kwa kutumia rangi. Na sehemu ya pili ilikuwa inahusu Biblia katika maigizo.Hiyo ni njia ya kuweka pamoja uzoefu binafsi wa maisha kwa kupitia kurasa za Injili. Pamoja na hayo mpango huo ni tunda la utume wa wafranciskani kati ya vjana ambao daima wamekuwa na tabia ya kusikiliza.
Hali kadhalika ndugu Matteo anafafanua zaidi akisema “hiyo ni kama safari ya kusindikizana ,kwa kufungua njia mpya ya maswali kwa vijana na pia kwa watu wazima wanao wakaribia na kuzidi hata  leo kutoa maswali yao.Ni njia mojawapo yenye nguvu ,na yenye maana kwa mambo mengi yanayotokea.Kuwakaribia vijana ,unaona nguvu  za mpango wa maisha yao , ambao ki ukweli unataka kwa dhati kujitokeza katika mwanga. Kujiweka katika safari na kutembea nao ni kuweza kuwasaidia wabadilike hata katika maswali yao , na hata wakati mwingine ni kuwapokea tu jinsi walivyo.

Hata hivyo hata wao wenyewe mara nyingine wanajitambua maisha yao na ndani ya mioyo yao. Wana uwezo wa kutambua kwamba kuna mtu aliye na uwezo juu yao ya kuwafanya wapende maisha yao , hadi kuwafikisha baadhi ya uchaguzi muhimu.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.