Kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la kuhudumua watoto duniani,UNICEF iliyotolewa
tarehe 28 Februari 2017 ya kwamba watoto na wanawake wakimbizi wahamiaji wanao kimbia
mateso mara kwa mara wanateseka kijinsia, unyanyasaji , kutumikishwa na kuwekwa vizuizi
wakati wa safari kupitia baharini kutoka Afrika ya Kaskazini na Italia.
Ikipatiwa jina safari ya hatari ya watoto kupitia njia ya wahamiaji ya Mediteranea,
ripoti hiyo inaeleza kwa kina hatari wanazokumbana nazo watoto wakimbizi wanaposafiri
kupitia jangwa la Sahara, Libya na hatimaye kuvuka bahari kuingia Italia.
Robo tatu ya watoto ya wakimbizi na wahamiaji waliohojiwa kwa ajili ya utafiti wanasema
wamekuwa wanakabiliwa na vurugu, unyanyasaji au mashambulizi katika mikono ya watu
wazima wakati wa safari hiyo.Wakati karibu nusu ya wanawake na watoto waliohojiwa
wanasema wamedhalilishwa kijinsia mara nyingi wakati wa kuhama kutoka sehemu moja
hadi nyingine, mara kadhaa na katika maeneo mbalimbali wanapofikia katika safari.
Wengi wa watoto wameripoti kuteswa kwa matusi au kisaikolojia, wakati nusu yao wamepata
mateso ya vipigo au aina nyingine ya unyanyasaji wa kimwili. Kwa upande wa wasichana,
wameonesha kuwa na matukio mengi zaidi ya kuliko wavulana.
Mwaka jana, watu wasiopungua 4,579 wamekufa wakijaribu kuvuka Mediterranean kutoka
Libya, na mmoja katika 40 ya wale ambao walijaribu na imekadiriwa kuwa watu 700 ambao
walipoteza maisha yao walikuwa ni watoto.Njia ya Kati ya Mediterranean, kutoka Afrika
Kaskazini kuelekea Ulaya, ndiyo watu wengi wanakufa kwa wingi na miongoni mwao zaidi
ni watoto na wanawake, anasema Afshan Khan Mkurugenzi wa Kanda na Mratibu Maalumu
wa UNICEF katika mgogoro wa Wakimbizi na Wahamiaji Ulaya.
Anaongeza "Tunaushawishi Muungano wa Ulaya utenge rasilimali kuimarisha mipango ya
ulinzi wa mtoto nchini Libya ili kuzuia watoto walio hatarini zaidi na pia kuinua
uwezo kwenye vituo vya mapokezi na malezi." Anaongeza akisema;njia hiyo inathibitiwa
na wafanya biashara haramu na watu wengine ambao wanawateka kwa urahisi kutokana na
kuwaona watoto na wanawake wamekata tamaa ,na kutafuta namna ya kukimbia kwa kutafuta
maisha bora
Mapendekezo mengine matano ni ulinzi wa watoto wakimbizi na wahamiaji wanaosafiri
peke yao, kuondokana na ushikiliaji watoto wanaosaka hifadhi, kuweka familia pamoja
kama njia ya kulinda watoto, kuchukua hatua dhidi ya vichochezi vya ukimbizi na uhamiaji.Anasisitiza
Afshan Khani kwamba mipango ya usalama na kisheria inahitajika kwa haraka ili kuwalinda
watoto wahamiaji , wawezekuwe kupata mahali pa usalama na kuwa mbali na wahalifu hao.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |