2017-02-28 13:57:00

Maombi ya msaada wa kifedha ili kujenga miji ya Ninawi Iraq


Maombi ya msaada wa kifedha  kwa ajili ya ujenzi wa mji na vijiji vya Piana na Ninawi ,mahali ambapo wanaishi wakristo walio kimbia vita vya wana jihadi wa dola ya Kiislam(Daesh) kati ya mwezi Juni na Agosti 2014.Maombi hayo yametolewa na Patriaki wa Wakaldayo kwasabu watu wake na wa jumuiya ya jamii nyingi waliacha ardhi yao ya jadi  na kusambaa katika maeneo mengi ya dunia. 
Maeneo ya kipatriaki na baadhi ya majimbo fulani tayari wamekusanya karibu milioni 500 dinari za Ira zenye thamani ya uro zaidi ya 380 elfu, ili kuharakisha ujenzi wa nyumba na makanisa yaliyo haribiwa wakati wa miaka ya vita vya kijihadi, kwa kufanya hivyo ni kuruhusu watu warudi wale wanao pendelea kurudi majumbani kwao.


Katika maombi ya Patriaki amewataka jumuiya zote kuendelea kusaidia kwa ukarimu mipango ya ujenzi kama walivyo kwisha fanya wakati wa kuwasaidia wakimbizi walio kimbia vijiji vya Ninawi .Taarifa inasema kwa njia hiyo waweze kuwahakikisha wale wanao taka kurudi nyuma wafike  kabla ya kuanza mwaka ujao.Halikadhalika ujumbe wa Partiaki wa kaldayo unatoa taadhali kwa waaangalizi wa kimataifa. Ni kwa dhamana ya kufuatilia kama inawezekana kutokea ukiukwaji na kuleta  migogoro kutoka kwa vikosi vinavyoshiriki vita dhidi ya majeshi ya kijihadi .Pia kuzuia mapigano baina ya serikali kuu na mikoa ya serikali ya Kurdistan ya Iraq katika mwelekeo wa kisiasa na utawala wa maeneo yaliyo chukuliwa hawali na wanajihadi.
Patriaki anasisitiza juu ya haja ya kuhusisha watu katika machakato wa ujenzi na makundi wa wenye sifa ambao wanatenda kwa moyo wa ukarimu na mshikamano bila kufuata maslahi yao binafsi.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.