2017-02-24 13:27:00

Usalama wa jamii ni muhimu kwanza katika kutafuta ujenzi wa amani.


"Matendo ya kimataifa ya Vatican kwa ajili ya amani" ni kauli mbiu ya Mkutano ambao Katibu Mkuu wa Sinodi ya maaskofu  Kardinali Lorenzo Baldisseri anamehutubia tarehe 24 Frbruari 2017 huko Roveto , ulioandaliwa na Chama cha Kazi ya Kengele wa mashujaa ambapo mwaka mada inatazama kwa kina juu ya waamuzi.
Kardinali Lorenzo Baldisseri anasema yoyote anayejishughulisha katika kazi ya kidplomasia anatambua vema ya kwamba  bila kuwa na matendo  ya kidiplomasia ya Vatican , waamini wengi na hata wasio kuwa wakatoliki, wanaweza kuona kizingiti katika uhuru wa dini.Na pia bila uwepo wa vatican katika mikutano mbalimbali ya nchi na kimataifa, kwa hakika inaweza kuonekana ukosefu wa uzoefu wa ushrikiano wa kibinadamu.Na maneno ya Papa Paulo wa VI , anasema kwamba matendo ya kuhakikisha kutokuwa na silaha , maelewano kati ya nchi na vilevile mapambano dhidi ya umasikini na aina zake , vinahitaji ujenzi kwanza wa amani.


Kwa hayo yote ni utambuzi zaidi kwa wale ambao wanajitoa katika utume wao kama wakleli katika huduma ya kidplomasia ya Vatican, kwa uwajibikaji ambao unawashirikisha katika shughuli za utume wa khalifa wa Mtume Petro , kama vile Baba Mtakatifu Francisko analivyosema, baada ya kukutana na wanadiplomasia septemba 2016 kwamba “katika kazi yenu , mnaitwa  kujikita  kila mtu kuleta huduma ya upendo kwa kile mnachowakilisha na kufanya moja wa  kusaidia ulinzi ambao  mko tayari  kuunga  mkono na siyo kusahihisha tu bali tayari kusikiliza kabla ya kutoa uamuzi , na kufanya hatua ya kuondoa mashaka na mvutano katika kuleta maelewano.Hayo ni maono wazi ambayo yanasisistizwa  kwa upande wa kazi ya Kanisa ya kidplomasia Vatican, ikiwa inakumbuka na kutazama wazi ule muungano wa pamoja ulio tolewa na Mtaguo wa Pili wa Vatican katika wosia wa Baba Mtakatifu  wa Mwanga wa mataifa,na kwa upande mwingine ni kuwa sehemu ya miendendo ya hali ya maisha ya kimataifa , lakini pia kwa mtazamo wa kuangalia lengo kubwa la uwelewa na maridhiano. 

 

Tunaweza kusema kwamba amani ya kweli katika nchi, kama alivyoeleza Mtakatifu Yohane XXIII katika wosia wake wa amani ya katika mataifa (“Pacem in Terris) maana yake ni kutoa ukamilisho wa historia ya wokovu.Hiyo ndiyo kusema kazi ya kidplomasia ya Vatican, maana yake ni kufanya kazi kama chombo cha amani. Katika uvumilivu na subira , kwa kuheshimu kanuni ,katika hali halisi , ambayo haki ya kimataifa inatoa kama msingi wa imani njema.Anaongeza Kardinali Baldisseri ,kuimarisha na kuhakikisha usalama ndiyo inabaki kupewa kipaumbele,na muhimu ili kuzuia sababu za migogoro zinazoweza kurejesha cheche za moto hata kama zilikuwa zimezisitishwa.


Vielelezo vya ukosefu wa haki viko mbele ya macho yetu wote ambapo husababisha hatari ya amani,kama vile  ukiukwaji wa haki,kama vile hukosefu wa chakula, afya,na elimu,ni baadhi lakini kwa ujumla kwa kuangalia wosia wa Baba Mtakatifu Francisko kuhusu utunzaji wa mazingira , nyumba ya wote masuala yote yametajwa , kwani tunagutuka kuona ya kwamba mabadiliko ya tabia nchi inazidi kuwa  hatari na kuasababisha maendeleo endelevu yazidi kuwa mbali katika ulimwengu wetu.








All the contents on this site are copyrighted ©.