Jumatatu 13 Februari ilikuwa ni "Siku ya radio duniani" ikiwa na kauli mbiu "Radio ni wewe" ambapo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO limetaka chombo hicho kitumiwe kuchagiza mashauriano. “Tunaishi katika mapinduzi ambamo tunabadilishana na kupata taarifa na bado katika mabadiliko haya, Radio imesalia kuwa muhimu na shirikishi”. Ni maneno ya Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Irina Bokova akitaka mapinduzi hayo sasa yachagize maendeleo endelevu.
Kila siku ni takaribani ya milioni 2,4 za watu duniani wana sikiliza radio Fm au kusikiliza
kwa kupitia mitandao ya intaneti.Kwa sasa kuna aina nyingi za kusikiliza radio kadri
miaka inavyozidi kupita ndivyo hata teknolojia, lugha inazidi kujionesha ukuaji wake
na kupata mapinduzi na hata kujionesha kwenye teknolojia mpya ya digital. Naye Profesa
wa historia ya Radio na Televisheni katika Chuo Kikuu Katoliki cha Milan nchini Italia
Giorgio Simonelli akihojiwa na mwandishi wa Habari wa Radio vatican anasema, Radio
ni chombo kinacho unganisha tabia kuu mbili ambazo tunafanya utafiti, tabia ya kijamii
na binafsi.Ni Radio ya kijamii kwa sababu leo hii unaweza kusikia radio unayo taka
hata kama huko nchi ya Austraria, kwa maana hiyo ni kujenga jumuiya kubwa inayozunguka
radio kwa njia ya kuchagua ambapo lakini ni uchaguzi binafsi. Zaidi Radio ni chombo
nyenye nguvu na utambulisho, kwani kila msikilizaji wa radio akitaka kuonesha ni radio
ipi anayosikiliza , jibu lake ni Radio yangu, hasemi televisheni yangu, kwa njia hiyo
ni kuthibitisha juu ya kumiliki binafsi radio.
Akieleza juu ya kauli mbiu iliyochaguliwa na Unisco “Radio ni wewe”, anasema hili
ni kama jina la kiini maacho, kwa ujumla matuminzi ya radio yamegunduliwa kwenye miaka
kati ya 60 na 70 ikiwa na kanuni zake hafifu, maana walitoa mambo rahisi sana , lakini
kwa wasikilizaji walijisikia kuhusika katika kuchagua nyimbo kama mtu alitaka kumtolea
wimbo kwa heshima ya mwingine.Baadaye ikatokea mtindo mwingine kama vile 3131 ,lengo
lilikuwa kumwezesha mtangazaji na msikilizaji waongee pamoja, maana kwanza ilikuwa
ni kutoa swali na baadaye mwingine kutoa mawazo yake kwa mjadala.Kwa upande wa watangazaji
wamekuwa wazi kutoa nafasi kubwa kwa wasikilizaji wao katika mijadala mbalimbali.
Akifafanua zaidi juu ya matumizi ya Radio Profesa Simonelli anasema mifano ya radio
kupitia mitandao, radio za vyuo vikuu vipindi maalumu kwa ajili ya michezo, vimekuwa
muhimu kwa wasikilizaji ,pia radio imekuwa daima huru kama chombo cha mawasiliano
hat kutoa ripoti za matukio mengi ya kijamii yasiyo takiwa.Aidha mfano kwa upande
wa Afrika Radio imesaidia sana katika kutoa taarifa muhimu za jamii, kwa mfano Stefano
Leszczynski anatukumbusha mmisionari wa Kikomboniani Padre Fabrizio Colombo mkurugenzi
wa Signis wa Shirika lisilo la Kiserikali lenye kuwa na wanachama washiriki 140 ambapo
wanashirikiana pamoja katika sekta ya Radio , televisheni, sinema , video , elimu
juu ya mitandao , inteneti na teknolojia mpya ya mawasiliano.
Aidha anasema kwamba katika uzoefu wake wa radio zaidi katika Afrika,ameona Radio
ni jambo linalo jikita katika mioyo ya watu wengi , na jinsi gani radio inaweza kubadili
hata maisha ya watu .Mfano kumhoji mtoto aliye nyanyaswa , anaweza kuleta mabadiliko
ya jamii katika nchi.Anatoa mfano wa miongoni mwa mambo aliyo yaona Afrika kuhusu
unyanyasaji wa watoto kama utumwa mamboleo,wazazi kuuza watoto wao, na kupotelea malishoni.Kwa
njia ya mahojianao ya watoto walio toroka au kupata manyanyaso mara baada ya kukataa
utii na kwa njia ya historia hiyo kupitia radio, inaweza kuokoa watoto wengi walio
kuwa wanakabiliwa na utumwa wa namna hiyo, hata kuiweka serikali kuwa macho katika
kukabiliana na utumwa na manyanyaso, hiyo ni mifano kuonesha jinsi gani Radio ni chombo
kilicho hai na kati cha kuweza kubadili hata maisha.
Hali kadhalika radio imebadili mamilioni ya watu walio kuwa wanasikiliza radio vatican
wakati wa vita vya Pili vya Dunia. Hasa ndugu wengi walio kuwa wamekimbia vurugu za
vita.Katika studia za Radio Vatican kwa miaka 6 mfululizo waliweza kutuma ujumbe
1,200,000 ambao ni zaidi ya masaa 12,000 ya matangazo.
Kama leo hii tunatazama maendele endelevu, na mabadiliko ni vema kumsikiliza kwa
shahuku kubwa Papa Pio wa XI tarehe 12 Februari 1931 wakati anafanya uzinduzi wa
Radio mbele ya mwanzilishi wa Radio Vatican Gugliermo Marconi akisema "Siri ya mpango
wa Mungu katika kufanikiwa kwa nafasi ya mitume mkuu ,kwa amri ya Mungu ili watu
wote wapate kuhabarishwa kwa njia ya mafundisho na mahubiri kwa kila kiumbe katika
mataifa ,na hasa kuanzia kwanza Marconi mahali ambapo tunaweza kufanya matumizi ya
uvumbuzi wa ajabu"
Sr Angela Rwezula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |