Ni kuendelea kufanya kazi kwa ushupavu kwa ajili ya amani na maridhiano , mazungumzo
kindugu kama wafuasi wa madhehebu mbalimbali. Ni maneno ya Askofu mkuu Angelo Becciu
aliyewakilisha Katibu wa Vatican kwenye maandimisho ya miaka 49 ya kuanzishwa kwa
Jumuiya ya Mtakatifu Egidio Mjini Roma.
Misa ya sherehe hizo iliadhimishwa katika Basilika ya Mtakatifu Yohane Laterano Ijumaa
10 Februari 2017, wakiwemo wanafunzi , wafanyakazi, wazee , watu wasio kuwa na makazi,
wakimbizi , wahamiaji , watu wakujitolea , marafiki na wahudumu wa Jumuiya ya Mtakatifu
Egidio Mkuu wa Shirika Marco Impagliazzo pamoja na mwanzilishi Andrea Riccardi
Uwepo hai wa ubunifu wa Kanisa la Roma , kwasababu hatua kwa hatua Jumuiya ya Mtakatifu
Egidio imeenea katika makanisa mengi ya ulimwengu, na kupanua kazi mbalimbali , na
siyo tu kijiografia , lakini pia katika mgawanyiko wa kazi na mipango mingi.Miradi
iliyopangwa haikupotea kwasababu anasema askofu Mkuu , kwa maongozi ya roho mtakatifu
mmeongeza ukarimu ambao ukawasaidiwa kufungua njia zaidi mpya na kupanua upeo wenu
kwa makanisa mengine.
Akitafakari juu ya masomo ya liturjia , Askofu Beciu anakumbuka mwanzo wa Jumuiya
ya Mtakatifu Egidio ilivyo jikita kwa watu wenye hali ya kubaguliwa na kutelekezwa.
Anasema walia waongozwa na somo kubwa kutoka kitabu cha mwanzo , mwanaume na mwanamke
ni viumbe katika mikono yake Mungu ,wao hubeba sura na mfano wa Mungu, na kwa njia
hiyo ni hadi ya binadamu. Aidha anabainisha kwamba mtazamo wa Muumba siyo ubaguzi
, hautenganishi katika makundi ya watoto wake: wao ni viumbe wake wapendwa , ambao
yeye yuko tayari kujitoa sadaka kwanjia ya mwanae mpendwa, kwasababu anawapenda kama
mtoto wake. Mbele ya binadamu mke , Mungu anatuonesha mashangao na kulipuka kwa kwa
kilio cha furaha .Kulingana na somo hilo Askofu Mkuu Becciu anasema ni kuonesha kwamba
kila mtu ni thamani kwa Bwana.
Askofu Becciu anatoa wito wa kuwa na mtazamo wa Muumba kwa kumtazama binadamu yeyote
wanaye kutana nao kama mwili mmoja na mfupa mmoja kwani binadamu yeyote anahitaji
uangailizi , na upendo wa Mungu ,kila mmoja aweze kumpokea mwingine kama zawadi kwa
maana huo ndiyo mkamilishano.Anaelezea shughuli mbalimbali za Jumuiya ya Mtakatifu
Egidio kwa watoto, watu pweke , masikini, kama wito wa Baba Mtakatifu Francisko juu
ya utume wa kwenda a kandoni kufanya umisionari katika pande zote za dunia , na hasa
sehemu zenye machafuko vurugu, mahali ambapo watu hawatambuliwi haki zao msingi. Kitendo
cha kwenda sehemu hizo kinarudisha uwepo wa Mungu katikati na kurudisha utu wa mtu
katika maisha ya jamii na maisha ya Kanisa.
Akitafakari juu ya Injili ya Mtakatifu Marko 7, 24-30, kuhusu mwanamke aliye kwenda
kuomba msaada kwa Yesu mtoto wake apone, Askofu anasema anajisikia kutoa pendekezo
la mfano wa mwanamke hasa anayetoka katika nchi ya Syria, na kufananisha na mwanake
huyo anayeombea huruma kwaajili ya binti yake.Hiyo ni kwasababu ,mwanamke wa Syria
anawakilishwa wanawake wengi wanaoomba msaada wa watoto wao. Wapo wanawake wengi duniani
wanao pata mateso kwaajili ya vita vurugu na ghasia . Mwanamke aliomba msaada wa Yesu
na alipofika nyumbani mtoto alikuwa amepona. Kwa njia hiyo ni kama jumuiya ya Mtakatifu
Egidio , kwa msaada wa Mungu wameweze kuchangia kupunguza mateso ya mama wengi wanao
teseka duniani
Mwisho askofu Becciu anazama Kanisa la Mtakatifu Yohane Lateran ambalo anasema ni
Mama Mkuu wa makanisa yote duniani.Kwa njia hiyo Jumuiya ya Mtakatifu Egido imenzaishwa
katika kanisa la Roma , na bado inaendelea kuwa muhimu wa uhalisia wa huduma katika
Kanisa. Kwa njia hiyo ni lazima kupenda mji na kushirikiana ili mji huo uweze kuwa
mzuri na wenye ukarimu.
Uhusiano wa askofu mkuu wa Roma ambaye na baba Mtaktifu francisko, unapaswa kuendelea
kwa tabia hiyo si kwaaajili ya mji huu peke yake bali ni upendo katika pande zote
za dunia . Na zaidi uzalendo wenu wa Roma uzidi kuwa na ushirikiano mkubwa na Baba
Mtakatifu Francisko ambaye anazidi kupanua moyo wake na mikono yake na kuwafikia sehemu
ambazo hawezi kufika yeye binafsi kimwili.
Kwa kufanya hivyo italeta maana ya kule mtu awe kitovu na kumfanaya kiala mmoja aliye
pemebezoni ajisikie kuwa kiini cha maisha yake mapya.Ni kwa njia hiyo tunaweza kuleta
mabadailiko ya dunia kijiografia na mbegu ya Injili onaweza kuzaa matunda tele ya
amani.
Alimazia Askofu Mkuu Becciu kwa kuwashauri warudie wito wa Baba Mtakatifu Francisko
alio utoa tarehe 15 Juni 2014 kwaajili yao ya kwamba endeleeni mbele katika njia hii
: sala , masikini na amani.Kwa kutembea katika njia hiyo msaidie kuongeza na kukuza
huruma katika mioyo ya jamii , ikiwa ni mapinduzi ya kweli ya amani,ile huruma na
upole , unao jengan a kukuza urafiki badala ya mizuka ya uadui na utofauti.
Sr Amgela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |